Friday, May 24, 2013

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI BARABARA YA IRINGA-DODOMA




Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa barabara ya Iringa –Dodoma itakapokamilika itasaidia kuinua uchumi wa mkoa wa Iringa na maeneo ya jirani na kuwataka wananchi kuhakikisha kuwa wanaitunza ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Kauli hiyo ameitoa leo mchana katika hotuba yake muda mfupi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Iringa-Dodoma Km 260 kwa kiwango cha lami katika eneo la Migoli.
 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha wageni


Dkt. Kikwete amesema kuwa kukamilika kwa barabara hiyo kutasaidia kuinua uchumi wa mikoa ya Iringa na Dododma na maeneo ya jirani kutokana na kuwa itafungia milango ya kibiashara kwa kurahisisha usafiri kwa abilia na usafirishaji wa mizigo. Akiongelea jukumu la wananchi katika kunufaika vizuri na ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, Rais Kikwete amewataka wananchi hao kijipanga katika kuongeza uzalishaji mali na kutumia vizuri fursa zilizopo ili kunufaika kiuchumi. 

Rais Kikwete amesema pamoja na minong’ono iliyopo kwa Serikali yake inatumia fedha nyingi sana klatika ujenzi wa barabara badala ya kupeleka fedha hizo katika maeneo mengine, amesema kuwa “kama taifa tumechelewa sana kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya barabara”. Amesema kuwa huo ni uamuzi wa makusudi wa kuwekeza kwa kasi katika miundombinu ya barabara ili kuweza kufungua fursa nyingine nyingi. Amesema kuwa lengo la Serikali ni kuunganisha kwa lami mtandao wa barabara zote nchini.  

Rais Dkt. Kikwete amekemea vikali tabia ya baadhi ya wananchi kuiba mafuta na vifaa mbalimbali katika miradi ya ujenzi wa barabara. Amesema kuwa wizi huo umekuwa ukirudisha nyuma muda wa utekelezaji na ukamilishaji wa miradi ya ujenzi wa barabara nchini. Amewataka wananchi kuwa walinzi dhidi ya wizi wa vifaa hivyo vya ujenzi na mafuta ili kuharakisha ujenzi ujenzi na ukamilishaji wa miradi hiyo.

Akimkaribisha Rais Kikwete kuhutubia, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli amepongeza mahusiano mazuri yanayofanywa na Rais Kikwete kwa wadau mbalimbali wa maendeleo jambo linalowezesha ujenzi wa mirandi mingi ya barabara nchini.
Dkt Magufuli ameseam kuwa mradi uliowekwa jiwe la msingi Iringa-Migori- Fufu Escarpment Km 189 unagharimu zaidi ya Tshs. Bilioni 164. 
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akipokea maelekezo ya mradi 

Akiongelea umakini katika kusimamia miradi ya ujenzi, Waziri wa Ujenzi amesema “Mkandarasi atakayezembea tutamfukuza” na msimamizi mshauri atakayeshindwa kuongoza atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
=30=