Saturday, September 24, 2011

MKUU WA MKOA WA RUVUMA AKABIDHIWA RASMI OFISI

  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe Said Thabit Mwambungu akisalimiana na watumishi wa ofisi yake mara baada ya kuwasili kwa mara ya kwanza kuanza kazi ya kuuongoza mkoa huo. Kulia kwake ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa, Dtk Anselm Tarimo


 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Said Thabit Mwambungu akisaini kitabu cha wageni katika ofisi yake mpya mara baada ya kuripoti kuanza kazi ya kuongoza shughuli za Serikali mkoani Ruvuma. Kushoto ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Dkt Christine Gabriel Ishengoma ambaye sasa ameahamia Mkoa wa Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Said Thabit  Mwambungu akipokea hati ya Makabidhiano ya ofisi kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Dkt Christine Gabriel Ishengoma tukio hilo lilishuhudiwa na wakuu wa sehemu na vitengo wote.

Picha zote kwa hisani ya Revocatus A. Kasimba, Msemaji wa Mkoa wa Ruvuma