Sunday, April 22, 2018

RAS Iringa yaiburuza 2-0 MUHAS Kamba



Timu ya kuvuta kamba ya RAS Iringa wanawake imeishinda timu ya kuvuta kamba ya MUHAS wanawake kwa mivuto 2-0. Katika mvutano wa aina yake uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mlandege na kushuhudiwa na mamia ya wapenda michezo wa mkoa wa Iringa na wageni kutoka sehemu mbalimbali waliofika mkoani hapa kwa ajili ya sherehe za Mei Mosi, 2018. 

Akiongea baada ya mvutano huo, Mratibu wa timu zote za RAS Iringa, Issa Matea alisema kuwa timu ya RAS Iringa maarufu kama Kisiki imepata ushindi huo kutokana na mshikamano na kujituma. Alitoa rai kwa timu washindani kuwa chonjo kwa sababu timu hiyo inalojukumu moja tu katika michezo hiyo. 

Alilitaja jukumu hilo kuwa ni kulinda heshima ya mkoa wa Iringa kwa kuibuka na ushindi katika mivuto yote katika michezo ya Mei Mosi, 2018.
=30=

No comments:

Post a Comment