Tuesday, June 2, 2015

DR. NCHIMBI AWATAKA WATUMISHI KUHAMIA WANGING'OMBE



Christopher Philemon - NJOMBE
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk.Rehema Nchimbi amewataka  watumishi walioamishiwa  na walioajiliwa katika halmashuri ya Wiaya ya Wanging’ombe   kuakikisha wamehamia kimakazi  katika wilaya hiyo.

Dk. Rehema Nchimbi,amesema kuwa wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe  watakiwa kupata huduma kutoka kwa watumishi hao na anashangaa kuona watumishi wanaishi Njombe mjini na kufanyakazi katika halmashuri ya wilaya ya Wanging’ombe ambayo ipo zaidi ya umbali wa kilometa 40 kutoka Njombe Mjini.

Nchimbi ametoa wiki mmoja toka leo kuakikisha watumishi hao wawe wameamia na kuishi katika Wilaya hiyo ili kuongeza ufanisi wa kazi na kuwa karibu na wananchi, aliyasema hayo kwenye ukumbi wa halmashuri ya wilaya ya Wang’ingombe wakati akifanya mkutano wa watumishi wa halmshauri hiyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Fedrick Mwakalebela  alisema kuwa Wilaya hiyo inamahitaji yote  muhimu kama vile ofisi, miundombinu ya maji na barabara  na kuwasihi watumishi hao wakikishe wanahamia katika wilaya hiyo haraka iwezekanazo kwani maendeleo ya Wanging’ombe yataletwa na wananchi wa Wanging’ombe kwa kushilikiana na watumishi. 

Mkurungenzi wa Wilaya hiyo Melizedeki Humbe alisema kuwa watumishi wengi katika wilaya hiyo bado wanaishi Njombe mjini lakini wamewaka mikakati ambayo ndani ya wiki mmoja waliopewa kuakikisha watumishi hao wote wanaamia katika wilaya hiyo mpya iliyo anzishwa mwaka 2012.
=30=



No comments:

Post a Comment