Tuesday, June 2, 2015

NJUWASA YAPOKEA BIL. 2.6 KUBORESHA HUDUMA YA MAJI NJOMBE




Christopher Philemon - NJOMBE

Mamlaka ya Maji Mkoa wa Njombe (NJUWASA)  imepokea kiasi cha fedha 2.6 ( 2,577,138,890.00)  bilioni  kutoka Wizara ya Maji  toka mwaka 2013 kwa ajili ya kuboresha hudumaya maji katika Mji wa Njombe.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mkoa wa Njombe Mhandisi, Daudi Majani amesema kuwa mpaka sasa fedha hizo zimetumika kujenga chanzo cha maji  cha Nyenga,matanti matatu ya maji na utandazaji wa mabomba ya maji ambapo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwisho wa mwezi wa saba mwaka huu.

Alisema kuwa mpaka sasa Ujenzi wa kidakio cha maji umekamilika  na ujenzi wa matanki matatu yaliyopo katika maeneo ya Airport, Kambalage, Igeleke na Nzengelendete  na kila tenki linauwezo wa ujazo wa lita 135,000 kila mojaHatua inayoendelea sasa ni utandazaji wa mabomba ya maji katika maeneo mbalimbali ya Mji wa Njombe.
Mradi huo ukikamilika utawezesha kufanya mji wa Njombe kuongeza upatikanaji wa maji kutoka  asilimia 55 hadi 80  na kufanya mji huo kuondoka na huwaba wa maji .

Majani amesema hayo jana kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Rehema Nchimbi alipotembelea vyanzo vya maji na kuangalia mtandao wa maji katika mji wa Njombe.

Mkuu huyo wa Mkoa amezitaka Halmashuri za Mji wa Njombe kushirikiana na mamlaka ya maji Mkoa wa Njombe kuakikisha wanatoa elimu kwa wananchi waliopo kwenye vyanzo vya maji ili kutunza vyanzo vya hivyo.
=30=





No comments:

Post a Comment