Tuesday, June 2, 2015

SEKTA YA MADINI KUINGIZA WATU 6,000 MKOANI NJOMBE



Christopher Philemon - NJOMBE
Zaidi ya wachina 6,000 wanatarajiwa kuingia katika Mkoa wa Njombe kwenye sekta ya madini hasa makaa ya mawe  na chuma kwenye eneo la Liganga na Mchuchuma wilayani Ludewa.

Hayo yamesemwa  jana kwenye Ukumbi wa Lutheran Makambako na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Rehema Nchimbi alipokuanaongea na watumishi wa Halmashuri ya Mji Makambako, alisema kuwa Mradi wa Linganga  na Mchuchuma unatarajiwa kuanza kuchimbwa makaa ya m awe na chuma hivi karibuni utatoa ajira zaidi ya 30,000 zikiwepo  za wazawa na wageni.

Kutokana na hilo amewataka watumishi wa Halmashauri ya Mji Makambako hasa sekta ya Ardhi kuakikisha wanaweka mipango mizuri ya matumizi ya ardhi na kupima viwanja ili kuwavutia wawekezaji mbalimbali katika ujenzi wa Hoteli za kisasa na halmashuri kuakikisha wanaboresha miundombinu ya Maji na barabara .

Dk. Nchimbi alisema kuwa mpaka sasa shirika la maendeleo ya Taifa (NDC) limeanza mchakato wa uthamini  wa mali za wananchi ili waweze kulipwa fidia kupisha mradi huo.

Aliwataka wananchi wa  Makambako na Njombe kwa Ujumla kujiandaa na ujio wa wageni mbalimbali kwa kufuga kuku, ng’ombe pamoja na mifugo mingine ili  kuweza kuwauzia wageni hao na kuongeza kipato cha familiya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako Hanana Chesco Mfikwa alisema kuwa  wanajiandaa kwa kuwapokea wageni hao kwa kuakikisha wanaweka mipango mizuri ambayo itasaidia wageni kuwekeza zaidi katika eneo la Makambako.
=30=

No comments:

Post a Comment