Thursday, August 16, 2012




UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WASHINGTON D.C.



UNAWALETEA  
SIKU YA MTANZANIA
Mahali: Tanzania House, 1232 22Nd Street, N.W. Washington D.C.; 20037                                   Tarehe: SEPTEMBA 15, 2012  Kiingilio: BURE                                                                                                                                                                                Muda: (Saa 4:00 asubuhi – Saa 12 Jioni)
Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Washington D.C. unawakaribisha Watanzania wote waishio  maeneo ya DMV (District of Columbia, Maryland na Virginia) na vitongoji vyake, kuhudhuria siku ya Mtanzania, ambapo Watanzania watashiriki kwenye kuonyesha bidhaa, tamaduni, mila na desturi za Kitanzania kwa wageni (Wamarekani na wa Mataifa mengine) watakaotembelea ubalozini.

Madhumuni makuu ya Ubalozi kuandaa Siku ya Mtanzania kwanza ni kuwaelimisha wenyeji wa Marekani kuhusu Tanzania. Pili kuitangaza zaidi Tanzania kwa kuvutia watalii wengi kutembelea Tanzania. Tatu ni kutambulisha na kutangaza biashara mbalimbali na huduma zitolewazo na Watanzania waishio hapa Marekani.

Ubalozi unaomba Watanzania wenye bidhaa mbambali za Kitanzania, mapishi (wenye leseni), vikundi vya ngoma, muziki, mitindo, na Watanzania wenye kampuni za utalii, kujiandikisha ubalozini kuanzia tarehe 1 hadi 15 Agosti, 2012 kwa maandalizi ya siku hiyo.

Kwa Watanzania watakaopenda kujitolea kushiriki siku hiyo au kuonyesha bidhaa mbalimbali wajiandikishe kwa wafuatao:
Dkt. Switbert Mkama 202 884 1087 au barua pepe smkama@tanzaniaembassy-us.org
Asia Dachi 202 884 1096 barua pepe adachi@tanzaniaembassy-us.org
Rosemary Mziray 202 884 1081 au barua pepe rmziray@tanzaniaembassy-us.org

Ubalozi unapenda kuwahamasisha Watanzania kuvaa vazi la Kitanzania.
Karibuni Wote.

No comments:

Post a Comment