Wednesday, July 24, 2013

TAFRIJA YA KUMPONGEZA LCPL ELIAS ADRIANO MBEGA KWA KUPANDISHWA CHEO



CPL William Kibasa (kushoto) na CPL Richard Mtove (kulia) wakifuatilia matukio ya hafla hiyo.

SGT Felister Maginga (kulia) na PTE Dorah Kibiki (kushoto) wakifuatia matukio ya hafla hiyo.





LCPL Elias Adriano Mbega akiwashukuru Maafisa, Snrnco Maaskari kwa kumuandalia tafrija ya kupandishwa cheo.



COL. SV. Shayo Mshauri wa Mgambo Mkoa wa Iringa akiteta jambo na CPL Goodluck Mwasubila.



LCPL Elias Adriano Mbega akifurahia hafla yake ya kupandishwa cheo.


CGT Felister Maginga akisalimia


CPL. Goodluck Mwasubila akibadilishana mawazo na Afisa Ugavi wa Mkoa Janeth Kitinye.





LCPL Elias Adriano Mbega akibadilishana mawazo na mate wake PTE. Dorah Kibiki.


Tuesday, July 23, 2013

SALAMU ZA RC IRINGA KATIKA MAZISHI YA MWANAJESHI ALIYEFARIKI DARFUR -SUDAN



Salamu za Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine G. Ishengoma (Mb.) katika mazishi ya CPL Osward Paulo Chaula amesema yafuatayo:
 

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine G. Ishengoma (Mb.) akitoa salamu za Mkoa wa Iringa

 Wanajeshi wakitoa heshima zao kwa marehemu CPL. Osward Paulo Chaula

Kwa masikitiko makubwa kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Iringa, napenda kutoa poke kwa familia ya Paulo Chaula kwa kufiwa na kijana wetu askari CPL.Osward Paulo Chaula, ambaye alikuwa akishiriki ulinzi wa amani nchini Darfur, Sudan.
Tukio hilo lilitokea tarehe 13 Julai, 2013.

Mkoa wa Iringa na Taifa kwa ujumla, tunakiri kwamba tumeondokewa na kijana wetu shujaa, mzalendona mchapa kazi ambaye umauti umemkumba akiwa kazini. askari huyu alikuwa tegemeo kubwa kwa Taifa letu la Tanznaia. Tunaahidi tutayaenzi yale yote mazuri aliyotuachia watanzania.
kutokana na tukio hilo, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilolo zinatoa pole ya Tshs. 500,000/= kwa familia ya Paulo Chaula.
=30=
MATUKIO KATIKA PICHA YA MAZISHI YA MWANAJESHI ALIYEFARIKI DARFUR NCHINI SUDAN 

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt Christine G. Ishengoma (Mb.) akisaini kitabu cha wageni katika mazishi ya CPL.Osward Paulo Chaula

 Baadhi ya waombolezaji wakipita kutoa heshima zao za mwisho mbele ya mwili wa marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Waombolezaji wakiomboleza kifo cha CPL.Osward Paulo Chaula

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akiaga mwili wa marehemu

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe. Gerald Guninita akiaga mwili wa marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa akiaga mwili wa marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakibeba jeneza lenye mwili wamarehemu wa CPL.Osward Paulo Chaula
Wanajeshi vijana wa JWTZ wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula ukipelekwa makaburini

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akiweka udongo katika kaburi alimolala marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi Scolastica Mlawi akiweka udongo katika kaburi alimolala marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Waombolezaji wakiomboleza kifo cha CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wa JWTZ wakiendelea na taratibu za kijeshi katika mazishi

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akiweka Shada la ua katika kaburi alimolala marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akikabidhi rambirambi kwa familia ya marehemu CPL.Osward Paulo Chaula




Sunday, July 21, 2013

MDAHALO WA FURSA ZA AJIRA KWA VIJANA WASOMI





TANGAZO LA MDAHALO
Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi isiyo ya kiserikali ya Community Integrated Communication and Culture (CICC) anawatangazia vijana wote wahitimu wa vyuo vikuu na wanaosoma katika vyuo vikuu nchini kujitokeza kushiriki katika mdahalo wa fursa za Ajira nchini.
MADA itakayojadiliwa ni Mchango wa Vijana wasomi katika upatikanaji wa Ajira nchini.
Mdahalo huo utafanyika katika ukumbi wa Highland, Iringa siku ya Jumanne tarehe 23/07/2013 kuanzia saa 4:00Asubuhi hadi saa 6:00 Mchana.
Vijana wote waliohitimu vyuo vikuu na wanaosoma katika vyuo vikuu nchini mnakaribishwa.
Mzungumzaji Mkuu katika Mdahalo huo atakuwa Mhe. Mch. Peter Msigwa- Mbunge wa Iringa Mjini.

HAKUNA KIINGILIO

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na;
Bi. Neema Mwamoto,
Mkurugenzi Mtendaji CICC
SLP 554, Iringa
Mob: 0752090900,























Friday, July 19, 2013

RC ATAKA JAMII ISHIRIKISHWE KATIKA UTUNZAJI WA BARABARA




Serikali mkoani Iringa imetaka jamii ishirikishwe ipasavyo juu ya dhana ya utunzani wa barabara ili kuhakikisha barabara zinadumu na kupitika muda wote. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akifungua kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Iringa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Dkt. Christine amesema “katika kuhakikisha tunakuwa na barabara zinazopitika muda wote, nimeona mapungufu ya ushiriki wa jamii juu ya utunzaji wa barabara hizo. Wananchi wamekuwa wakifanya shughuli ndani ya hifadhi ya barabara na kuacha uchafu kwenye barabara na uchafu huo kuziba mifereji na kuharibu barabara”. Aidha, amewataka wajumbe wa kikao hicho kutoa elimu kwa wananchi ili washiriki kikamilifu katika utunzaji wa barabara hizo ili ziweze kudumu na kuwahudumia kwa muda mrefu. Amesema kuwa uchafu unaharibu mazingira, unaziba mifereji ya barabara na kusababisha mafuriko kwenye makazi ya wananchi.

Mkuu wa mkoa wa Iringa ametoa rai kwa viongozi na wananchi kushirikiana na miradi ya ujenzi na ukarabati wa barabara ya Iringa –Dodoma na Iringa-Mafinga. Amesema kuwa ushirikiano huo na elimu kwa wananchi utasaidia kukomesha hujuma za wizi hasa wa mafuta na ementi ili miradi hiyo iweze kuwa ya manufaa kwa mkoa wa Iringa na taifa kwa ujumla na kukamilika kwa muda muafaka.

Aidha, amewataka wajumbe hao kuendela kushirikiana katika kutoa elimu kwa wananchi juu ya Sheria mpya ya hifadhi ya barabara ambayo ni mita 30 kil upande kutoka katikati ya barabara. Amesema “wananchi waendelee kuelimishwa juu ya umuhimu wake kwani wanapojenga na kubomolewa nyumba zao haipendezi. Inawagharimu na kuwaumiza sana” alisisitiza Mkuu wa mkoa wa Iringa.
=30=