Friday, August 19, 2011

TANI MIL 1.4 ZAONGEZEKA MAZAO YA CHAKULA NA BIASHARA IRINGA
Mkoa wa Iringa umefanikiwa kuongeza kilimo cha mazao ya chakula na biashara hadi kufikia tani milioni 1.4 katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru.

Kaimu Katibu Tawala Msaidize, Sehemu ya Uchumi na Sekta za Uzalishaji, Shenal S. Nyoni akifafanua jambo

Akiwasilisha taarifa ya mafanikio ya kilimo katika miaka 50 ya Uhuru, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Uchumi na Sekta za Uzalishaji, Shenal Nyoni katika Iringa Day iliyofanyika katika ukumbi wa JKT ndani ya uwanja wa John Mwakangale Uyole, Mbeya yanapofanyika maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Nyoni amesema “katika miaka ya 60 mkoa ulikuwa ukizalisha tani laki 3.05 za mazao hayo na hadi kufikia mwaka 2011 mkoa umefanikiwa kizalisha tani milioni 1.4”.

Amesema katika sekta ya uvuvi mkoa una mabwawa 4,167 yanayozalisha tani 1,449 za Samaki na kuuingizia shilingi bilioni 4.3 kwa mwaka.
Nyoni amesema kuwa mkoa pia ulishiriki katika mashindano ya mifugo ya Afrika Mashariki na kuchukua nafasi ya kwanza. Katika mashindano hayo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ndiyo ilichukua ushindi huo.

Akiongelea sekta ya viwanda amesema mkoa una viwanda vya kusindika na kuyaongezea mazao thamani. Mkoa una viwanda vikubwa vinne, viwanda vya kati 53 na 66 ni viwanda vidogo na mashine 1,992 za kusaga nafaka.

Awali akitoa salamu zake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema kuwa mkoa wa Iringa umefanikiwa kuzalisha chakula cha kuutosheleza mkoa kwa sehemu kubwa na kuonesha masikito yake kwa baadhi ya sehemu zinazokabiliwa na upungufu wa chakula kutokana na upungufu mkubwa na ukame ulioyakabili baadhi ya maeneo hayo.

Amesema mkoa umalima mazao mengi yakimo mazao ya biashara kama mbao, chai, pareto, kahawa, alizeti na maua.

No comments:

Post a Comment