Saturday, October 8, 2011

MUFINDI WASHAURIWA KUANZISHA CHUO KIKUU

Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewashauri wanamufindi kuangalia uwezekano wa kuwa na chuo kikuu ili kuwasogezea karibu huduma hiyo muhimu wananchi.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akiongea na watumishi wa Serikali kuu, Halmashauri na taasisi mbalimbali katika ukumbi mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi.
Karibu Wilayani Mufindi, Mhe. Mkuu wa Mkoa
Dkt. Ishengoma amesema “pamoja na kuwa na mafanikio makubwa katika nyanja za uzalishaji na uchumi, Mufindi tufikirie kuwa na chuo kikuu”. Amesema kuwa chuo kikuu ni muhimu sana katika kuzalisha wanataaluma watakaosaidia kusukuma zaidi gurudumu la maendeleo Wilayani hapo. Amesema uanzishwaji wa chuo kikuu Wilayani Mufindi utawasaidia wananchi wengina wa maeneo ya jirani kuvutika katika kujiendeleza kielimu.
Akiongelea sekta ya maji, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa sekta hiyo bado inaasilima zilizo chini jambo linalowakoshesha wananchi wengi huduma hiyo. Amesema “kwa pamoja ni lazima tujitahidi ili kuongeza kasi ili tufikie malengo ya matakwa ya sera ya maji”.
Aidha, ameishauri Halmashauri hiyo kuangalia vyanzo vingine vinavyoweza kuiletea mapato ili kuiwezesha Halmashauri hiyo kujiendesha vizuri zaidi. Amesema kuwa Halmashauri inapojiimarisha kimapato inapanua wigo wake wa utoaji huduma kwa wananchi na kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.
Akiwasilisha taarifa ya Wilaya ya Mufindi kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bibi. Evarista Kalalu amesema kuwa ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400, wilaya yake imeongeza miradi ya maji na kuongeza idadi ya watu wenye uwezo wa kupata maji safi na salama kutoka asilimia 40 mwaka 2005/2006 kwa wakazi wa mjini, hadi asilimia 53 mwaka 2010/2011. Aidha, idadi imeongezeka kutoka asilimia 56 mwaka 2005/2006 kwa wakazi wa vijijini, hadi asilimia 61 mwaka 2010/2011.


Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bibi. Evarista kalalu akisisitiza jambo

Amesema kuwa miradi hiyo ni ya uchimbaji wa visima 35 ambavyo vimewapatia maji wananchi wapatao 8,750 pamoja na ujenzi wa mtego mmoja wa maji ambao unawanufaisha wananchi 2000.
Bibi. Kalalu amesema kuwa uhifadhi wa vyanzo vya maji na rasilimali za maji umeongezeka kutoka vyanzo 100 vilivyokuwa vimehifadhiwa mwaka 2005 hadi kufikia vyanzo 705 mwaka 2010.  Amesema vyanzo hivyo ni vile ambavyo hutiririsha maji yake katika mto wa Ruaha.

No comments:

Post a Comment