Tuesday, February 20, 2018

SERIKALI YATOA MASHARTI MATATU KUFUNGULIWA NGODI WA NYAKAVANGALA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Serikali yatoa masharti matatu kufungua mgodi wa kuzalisha dhahabu Nyakavangala na kuelekeza yatekelezwe ndani ya wiki mbili.

Masharti hayo ambayo ni kupitisha kanuni za uchimbaji madini, wataalam kutoka wizara ya madini kukagua mashimo yote ya kuchimba dhahabu na mafunzo ya usalama katika machimbo yalitolewa na naibu waziri wa Madini, Dotto Biteko aliyefanya ziara ya siku moja katika mgodi wa Nyakavangala uliopo katika Kata ya Malengamakali wilayani Iringa jana.
 
Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko (Mb)
Biteko alisema kabla ya kufunguliwa mgodi huo mambo hayo matatu lazima yafanyiwe kazi ili kufanya mazingira ya uchimbaji dhahabu kuwa salama. Katika kuhakikisha mazingira yanakuwa sawa, aliwataka wachimbaji hao kuwa wakweli na wazalengo kwa nchi yao katika kiasi cha dhahabu kinachozalishwa mgodini hapo. Akiongelea utoroshaji madini hayo, alisema “mchimbaji anayedhani serikali ya Dr. John Magufuli anaweza kutorosha dhahabu atafute kazi nyingine” alisema Biteko. 

Aliongeza kuwa serikali ipo makini kuhakikisha madini hayo yanawanufaisha watanzania na kuchangia katika uchumi wa Taifa.

Awali mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa katika kuhakikisha hali ya machimbo dhahabu ya Nyakavangala inakuwa salama, kamati ya ulinzi na usalama Mkoa wa Iringa iliagiza ufanyike ukaguzi katika mashimo yote yanayochimba dhahabu katika mgodi huo. Alisema lengo la ukaguzi huo ni kuwahakikishia usalama wachimbaji hao na kuepuka vifo vitokanavyo na mashimo hayo kuanguka.
=30=

No comments:

Post a Comment