Friday, October 16, 2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MWENENDO WA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI ILIYOTOLEWA NA MKUU WA MKOA WA IRINGA MHESHIMIWA AMINA MASENZA TAREHE 16/10/2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU
MWENENDO WA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI
ILIYOTOLEWA NA MKUU WA MKOA WA IRINGA MHESHIMIWA AMINA MASENZA TAREHE
16/10/2015
1.0 Utangulizi
Mkoa
wa Iringa unaendelea na maandalizi mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha Uchaguzi
Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 25/10/2015. Maandalizi
hayo ni pamoja na Wagombea kuendelea na kampeni kunadi sera zao, mafunzo kwa
watendaji, maandalizi ya vituo vya kupigia kura, uhakiki wa taarifa zilizomo
kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na mapokezi ya vifaa.
2.0 Hali ya Kampeni za Uchaguzi
Kampeni
za uchaguzi zilianza rasmi tarehe 22/08/2015 na zitaendelea hadi tarehe
24/10/2015. Ratiba za kampeni zimeandaliwa na Wasimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi
Wasaidizi wa Uchaguzi kwa kuvishirikisha vyama vya siasa. Kwa ujumla Kampeni
hizo katika mkoa wa Iringa zinaendelea kwa hali ya amani na utulivu.
3.0 Kamati za Maadili
Wasimamizi
wote wa Uchaguzi wa Majimbo ya Uchaguzi wameunda Kamati za Maadili katika ngazi
ya Jimbo. Kamati hizo pia zimeundwa katika ngazi ya Kata kwa Kata zote za Mkoa
wa Iringa. Lengo la kuundwa kwa Kamati hizi ni kusimamia utekelezaji wa maadili
ya Uchaguzi ya mwaka 2015.
4.0 Mafunzo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi
Mafunzo
tayari yametolewa kwa Wasimamizi wa uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Mafunzo hayo yalitolewa kwa Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa
Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika ngazi ya Jimbo. Aidha, Halmashauri
zimeendesha mafunzo pia kwa Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya Kata zote za Mkoa wa
Iringa kuanzia tarehe 3/10/2015 hadi 13/10/2015.
5.0 Utangazaji wa nafasi za Wasimamizi
wa Vituo, Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo,
na Makarani waongozaji
Matangazo
hayo yalitolewa katika Halmashauri zote 5 za Mkoa wa Iringa tarehe 1/10/2015
hadi 5/10/2015. Zoezi linaloendelea ni kufanya uchambuzi wa walioomba nafasi
hizo ili kupata wenye sifa stahiki.
6.0 Vituo vya Kupigia Kura
Awali
Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitoa orodha ya vituo 1,641 vitakavyotumika katika
zoezi la upigaji kura kwa Mkoa wa Iringa kwa Halmashauri zote 5. Idadi hiyo
imepungua kufikia vituo 1,601 baada ya uhakiki wa wapiga kura kwenye Daftari la
Kudumu la Wapiga Kura unaoendelea kufanywa na Wasimamizi wa Uchaguzi.
7.0 Mapokezi ya Vifaa
Halmashauri
zimepokea vifaa kama masanduku, mifuniko, Tshirts, kofia, Vituturi, na fomu mbalimbali kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu.
Aidha,
Wasimamizi wanaendelea kufanya tathmini ili kujiridhisha endapo
vifaa vilivyopokelewa vinakidhi mahitaji.
8.0 Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
Tayari
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetoa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa
Halmashauri zote. Kazi inayoendelea hivi
sasa ni uhakiki wa idadi ya wapiga kura kwa kila kituo.
9.0 Mambo Muhimu ya Kuzingatiwa na
Wapiga Kura na Wananchi
(a) Sifa
za Mpiga Kura
- Mpiga kura ni raia yeyote wa Tanzania,
- Aliyefikisha umri wa miaka 18,
- Aliyeandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,
- Mwenye kadi ya kupigia kura iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
- Lazima awe Mkazi wa eneo analotaka kupiga kura na jina lake limeorodheshwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura au Orodha iliyobandikwa katika Kituo cha Kupigia Kura.
- Orodha ya Wananchi wanaoshahili kupiga kura itabandikwa kwenye Vituo husika siku 8 kabla ya Uchaguzi hivyo wananchi wapitie Orodha hiyo mapema ili wajue vituo watakavyopigia kura.
- Vituo vyote vya kupigia kura havitawekwa katika nyumba za watu binafsi, vituo vidogo vya Polisi wala nyumba za Ibada kwa lengo la kuwapa nafasi na uhuru wapiga kura.
- Katika zoezi la Kupiga Kura kipaumbele kitatolewa kwa watu wenye Ulemavu, Wanawake Wajawazito na wale wenye Watoto Wachanga, Wagonjwa na Wazee ili wasikae muda mrefu kwenye mistari.
- Wapiga kura wasioweza kupiga kura wao wenyewe, wasioona au wasiojua kusoma watasaidiwa na watu watakao wateua wao wenyewe. Aidha, Tume imeandaa kifaa (Tactile Ballot Folder) kitakachowasaidia wapiga kura wasioona ili waweze kupiga kura zao wao wenyewe.
- Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na vitafungwa saa 10.00 Jioni, iwapo kutakuwa na wapiga kura katika mistari muda huo, wapiga kura hao wataruhusiwa kupiga kura. Aidha, wapiga kura watakaofika baada ya muda huo hawataruhusiwa kupiga kura.
10.0 Makosa ya Uchaguzi (Makosa ya
Jinai kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Sura 343 na Sheria ya Uchaguzi wa
Serikali za Mitaa Sura 292)
- Kujaribu kupiga kura wakati muda wa kupiga kura umekwisha,
- Kujaribu kupiga kura wakati hauruhusiwi kisheria kupiga kura,
- Kujaribu kupiga kura zaidi ya mara katika uchaguzi,
- Kujaribu kupiga kura kwa kutumia kadi ya mtu mwingine,
- Kuweka kitu kingine zaidi ya karatasi ya kupigia kura katika sanduku la kuhifadhia kura.
- Kuchana orodha ya wapiga kura au mabango yoyote ya elimu kwa mpiga kura.
- Kughushi au kuharibu karatasi ya kura,
- Kuchapisha na kusambaza karatasi za kura bila mamlaka kisheria,
- Kupokea au kutoa rushwa kabla na wakati wa uchaguzi,
- Kumzuia mtu kupiga kura yake kwa uhuru na amani,
- Kutoa siri ya mpiga kura mwenzio kuwa anakwenda kumpigia kura Fulani au amempigia mtu Fulani.
- Kuvaa au kuonesha alama yoyote ya chama wakati wa zoezi la upigaji kura.
- Kuchukua kadi za Wapiga Kura ili wasiweze kupiga Kura.
- Kutumia vitisho na nguvu kuwashawishi wapiga kura ili wakupigie kura.
11.0 Ulinzi na Usalama
Mkoa
wa Iringa umejipanga vizuri kuhakikisha amani na usalama kwa kipindi chote cha
kampeni za Uchaguzi na wakati wa zoezi la kupiga kura vyote vinafanyika vizuri
kwa mujibu wa ratiba na kwa kuzingatia sheria za nchi ili Wananchi waendelee
kuwa salama na kutekeleza majukumu yao.
Napenda
kutoa rai kwa wananchi wote wa Mkoa wa Iringa kufahamu na kukubaliana kuwa yapo
maisha na yataendelea kuwepo hata baada ya Uchaguzi Mkuu hapo tarehe 25 Oktoba,
2015. Hivyo, kila mmoja wetu lazima atimize wajibu wake katika kuhakikisha
amani na utulivu vinaendelea kuwepo katika kipindi hiki chote ili tumalize
zoezi hili tukiwa wamoja na wenye mshikamano mkubwa.
Katika
kuhakikisha mkoa unakuwa na utulivu kwa kipindi chote, nimekutana na makundi
mbalimbali kujadili suala la amani kuelekea Uchaguzi Mkuu. Makundi hayo ni
viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa madhehebu ya dini, wazee na watu wenye
ushawishi katika jamii na waandishi wa habari.
Lengo
ni kupata maoni yao na ushauri wa jinsi ya kufanikisha Uchaguzi Mkuu kwa amani
na utulivu.
Napenda
kuchukua nafasi hii kuwathibitishia Wananchi wa Mkoa wa Irirnga kuwa, ulinzi
utakuwepo wa kutosha katika kipindi chote cha kampeni na siku ya kupiga kura
tarehe 25/10/2015.
Jeshi
la Polisi limejipanga vizuri kuwalinda wananchi wote, hivyo, rai yangu kwa Wananchi
ni kuwa jitokezeni kwa wingi siku ya kupiga kura mapema na baada ya kupiga kura
rudini kwenye maeneo yenu kuendelea na shughuli nyingine. Wananchi wasibaki
kwenye vituo vya kupigia kura baada ya kupiga kura.
Asanteni kwa kunisikiliza
Wednesday, September 23, 2015
TASAF WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UWAZI NA UWAJIBIKAJI
Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kulipa uzito tatizo
la utapiamlo ili kupunguza udumavu, ulemavu na vifo vya watoto na wanawake
wanaonyonyesha.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa
wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua mkutano wa kamati za lishe za
halmashauri na mkoa wa Iringa kuhusu
masuala ya lishe ya mama na mtoto katika ukumbi wa Veta.
Masenza alisema “matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata
kuua watoto wetu na wanawake hasa wale wajawazito na wanaonyonyesha. Pia jamii
kwa ujumla imekuwa ikiathirika kwa njia moja au nyingine kwa kuwepo kwa
utapiamlo”. Masenza aliongeza “pamoja
na maendeleo ambayo nchi yetu imeyapata katika maeneo mbalimbali, bado tatizo
la lishe duni linaendelea kuathiri uchumi na kuchangia kuwepo kwa umasikini.
Lishe duni pia huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili hivyo
kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na taifa”.
Alisema kuwa uboreshaji wa hali ya
lishe nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na
kupunguza umasikini kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Aliongeza kuwa kwa
upande wa watoto lishe husaidia kuongeza uwezo wao kiakili na usanisi shuleni.
Mkurugenzi wa Mwanzo bora Dkt. Daniel
Nyagawa alilitaja lengo kuu la mradi huo kuwa ni kuisaidia serikali katika
kutekeleza mkakati wa taifa wa lishe pamoja na mkakati wa taifa wa kubadili
tabia na mienendo ya maisha.
Aliongeza kuwa mradi wa lishe wa
mwanzo bora unalenga kupunguza upungufu wa damu kwa wajawazito na wanawake
wanaonyonyesha kwa asilimia 20. Aidha, unalenga kupunguza udumavu kwa watoto
chini ya umri wa miaka miwili kwa asilimia 20. Mwisho mradi unalenga kujengea
uwezo wa utekelezaji kwa serikali mashirika yasiyo ya kiserikali na kijamii.
Dkt. Nyagawa alisema kuwa mradi
unatumia mkakati wa mawasiliano yanayolenga kubadili tabia katika masuala ya
lishe. Alisema kuwa mradi unalenga tabia ambazo zikifuatwa zitaleta matokeo
makubwa katika kupunguza udumavu na upungufu wa damu. Aliongeza mradi unalenga
kubadilisha tabia binafsi ambazo zamani miradi mingi haikufanya.
Akiongelea walengwa wa mradi huo,
Dkt. Nyagawa aliwataja “walio ndani ya siku 1,000 tangu kutungwa kwa mimba hadi
mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili”.Alifafanua kuwa ni mama mjamzito,
anayenyonyesha na mama mwenye mtoto umri usiozidi miaka miwili. Baba ambaye
mwenza au mke wake ana sifa zilizotangulia na wale wote wanaolea watoto wenye
umri usiozidi miaka miwili.
Mradi wa lishe wa mwanzo bora ni
mradi wa lishe uliofadhiliwa na serikali ya marekani kupitia USAID ukitekelezwa
katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Dodoma, Manyara na Mbeya.
=30=
JAMII YATAKIWA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO IRINGA
Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kulipa uzito tatizo
la utapiamlo ili kupunguza udumavu, ulemavu na vifo vya watoto na wanawake
wanaonyonyesha.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa
wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua mkutano wa kamati za lishe za
halmashauri na mkoa wa Iringa kuhusu
masuala ya lishe ya mama na mtoto katika ukumbi wa Veta.
Masenza alisema “matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata
kuua watoto wetu na wanawake hasa wale wajawazito na wanaonyonyesha. Pia jamii
kwa ujumla imekuwa ikiathirika kwa njia moja au nyingine kwa kuwepo kwa
utapiamlo”. Masenza aliongeza “pamoja
na maendeleo ambayo nchi yetu imeyapata katika maeneo mbalimbali, bado tatizo
la lishe duni linaendelea kuathiri uchumi na kuchangia kuwepo kwa umasikini.
Lishe duni pia huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili hivyo
kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na taifa”.
Alisema kuwa uboreshaji wa hali ya
lishe nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na
kupunguza umasikini kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Aliongeza kuwa kwa
upande wa watoto lishe husaidia kuongeza uwezo wao kiakili na usanisi shuleni.
Mkurugenzi wa Mwanzo bora Dkt. Daniel
Nyagawa alilitaja lengo kuu la mradi huo kuwa ni kuisaidia serikali katika
kutekeleza mkakati wa taifa wa lishe pamoja na mkakati wa taifa wa kubadili
tabia na mienendo ya maisha.
Aliongeza kuwa mradi wa lishe wa
mwanzo bora unalenga kupunguza upungufu wa damu kwa wajawazito na wanawake
wanaonyonyesha kwa asilimia 20. Aidha, unalenga kupunguza udumavu kwa watoto
chini ya umri wa miaka miwili kwa asilimia 20. Mwisho mradi unalenga kujengea
uwezo wa utekelezaji kwa serikali mashirika yasiyo ya kiserikali na kijamii.
Dkt. Nyagawa alisema kuwa mradi
unatumia mkakati wa mawasiliano yanayolenga kubadili tabia katika masuala ya
lishe. Alisema kuwa mradi unalenga tabia ambazo zikifuatwa zitaleta matokeo
makubwa katika kupunguza udumavu na upungufu wa damu. Aliongeza mradi unalenga
kubadilisha tabia binafsi ambazo zamani miradi mingi haikufanya.
Akiongelea walengwa wa mradi huo,
Dkt. Nyagawa aliwataja “walio ndani ya siku 1,000 tangu kutungwa kwa mimba hadi
mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili”.Alifafanua kuwa ni mama mjamzito,
anayenyonyesha na mama mwenye mtoto umri usiozidi miaka miwili. Baba ambaye
mwenza au mke wake ana sifa zilizotangulia na wale wote wanaolea watoto wenye
umri usiozidi miaka miwili.
Mradi wa lishe wa mwanzo bora ni
mradi wa lishe uliofadhiliwa na serikali ya marekani kupitia USAID ukitekelezwa
katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Dodoma, Manyara na Mbeya.
=30=
WANAWAKE IRINGA WATAKIWA KUPIMA SARATANI YA KIZAZI
Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wanawake mkoani Iringa wametakiwa
kujitokeza kupima saratani ya mlango wa kizazi ili wanapogundulika na saratani
hiyo waanze matibabu mapema.
Wito huo umetolewa na mganga mkuu wa
mkoa wa Iringa, Dkt. Robert Salim alipokuwa akifungua semina ya kufuatilia
utekelezaji wa mipango na maazimio yaliyowekwa kuhusu kukabiliana na saratani
ya mlango wa kizazi iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha afya ya msingi mjini
Iringa.
Dkt. Salim alisema kuwa saratani ya
mlango wa kizazi inasababisha maradhi na vifo kwa wanawake wengi nchini isipotambuliwa
na kuanza kutibiwa mapema. Alisema kuwa wanawake wote walioanza mahusiano ya
kimapenzi wanatakiwa kujitokeza katika vituo vya afya kupima ili
wanapogundulika wameathirika na saratani hiyo waanze tiba mapema. Alisema kuwa
yapo mahusiano makubwa baina ya maambukizi ya virusi vya ukimwi na saratani ya
mlango wa kizazi. Kutokana na mahusiano hayo ambayo kwayo mkoa wa Iringa
umeathirika sana na maambukizi ya ukimwi kwa 9.1% hivyo kusababisha ugonjwa wa
saratani ya mlango wa kizazi kuwa juu.
Nae Mkurugenzi wa uboreshaji afya
kutoka taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Dkt. Sarah Maongezi alisema kuwa
semina hiyo ililenga kufuatilia utekelezaji wa mipango na maazimio ya awali
waliyojiwekea katika kukabiliana na tatizo la saratani ya mlango wa kizazi
mkoani hapa. Alisema kwa kuwa mkoa wa Iringa ulianza muda mrefu mapambano dhidi
ya saratani ya mlango wa kizazi hivyo mkoa unatakiwa kuwa umepiga hatua za
mafanikio zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine nchini. Alisema kuwa kwa hatua
iliyofikiwa na mkoa wa Iringa, mkoa huo unaweza kujihamasisha kununua vifaa na
vifaa tiba kwa lengo la kukabiliana na saratani ya mlango wa kizazi.
Saratani ya mlango wa kizazi ni
miongoni mwa magonjwa yanayosababisha vifo kwa wanawake wengi ikikadiriwa kuwa
zaidi ya wanawake 4,000 hupoteza maisha nchini kila mwaka.
=30=
Subscribe to:
Posts (Atom)