Friday, October 16, 2015

MATUKIO KATIKA PICHA YA PRESS CONFERENCE IRINGA











TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MWENENDO WA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI ILIYOTOLEWA NA MKUU WA MKOA WA IRINGA MHESHIMIWA AMINA MASENZA TAREHE 16/10/2015



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MWENENDO WA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI ILIYOTOLEWA NA MKUU WA MKOA WA IRINGA MHESHIMIWA AMINA MASENZA TAREHE 16/10/2015

1.0 Utangulizi
Mkoa wa Iringa unaendelea na maandalizi mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 25/10/2015. Maandalizi hayo ni pamoja na Wagombea kuendelea na kampeni kunadi sera zao, mafunzo kwa watendaji, maandalizi ya vituo vya kupigia kura, uhakiki wa taarifa zilizomo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na mapokezi ya vifaa.  
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza (kulia) na Katibu Tawala wa Mkoa Wamoja Ayubu
2.0 Hali ya Kampeni za Uchaguzi
Kampeni za uchaguzi zilianza rasmi tarehe 22/08/2015 na zitaendelea hadi tarehe 24/10/2015. Ratiba za kampeni zimeandaliwa na Wasimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kwa kuvishirikisha vyama vya siasa. Kwa ujumla Kampeni hizo katika mkoa wa Iringa zinaendelea kwa hali ya amani na utulivu. 

3.0 Kamati za Maadili
Wasimamizi wote wa Uchaguzi wa Majimbo ya Uchaguzi wameunda Kamati za Maadili katika ngazi ya Jimbo. Kamati hizo pia zimeundwa katika ngazi ya Kata kwa Kata zote za Mkoa wa Iringa. Lengo la kuundwa kwa Kamati hizi ni kusimamia utekelezaji wa maadili ya Uchaguzi ya mwaka 2015.

4.0 Mafunzo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi
Mafunzo tayari yametolewa kwa Wasimamizi wa uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Mafunzo hayo yalitolewa kwa Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika ngazi ya Jimbo. Aidha, Halmashauri zimeendesha mafunzo pia kwa Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya Kata zote za Mkoa wa Iringa kuanzia tarehe 3/10/2015 hadi 13/10/2015. 

5.0 Utangazaji wa nafasi za Wasimamizi wa Vituo, Wasimamizi Wasaidizi  wa Vituo, na Makarani waongozaji  
Matangazo hayo yalitolewa katika Halmashauri zote 5 za Mkoa wa Iringa tarehe 1/10/2015 hadi 5/10/2015. Zoezi linaloendelea ni kufanya uchambuzi wa walioomba nafasi hizo ili kupata wenye sifa stahiki.

6.0 Vituo vya Kupigia Kura
Awali Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilitoa orodha ya vituo 1,641 vitakavyotumika katika zoezi la upigaji kura kwa Mkoa wa Iringa kwa Halmashauri zote 5. Idadi hiyo imepungua kufikia vituo 1,601 baada ya uhakiki wa wapiga kura kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaoendelea kufanywa na Wasimamizi wa Uchaguzi.  

7.0 Mapokezi ya Vifaa
Halmashauri zimepokea vifaa kama masanduku, mifuniko, Tshirts, kofia, Vituturi, na fomu mbalimbali kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu. 
Aidha, Wasimamizi wanaendelea kufanya tathmini ili kujiridhisha  endapo  vifaa vilivyopokelewa vinakidhi mahitaji.

8.0 Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
Tayari Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetoa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Halmashauri zote.  Kazi inayoendelea hivi sasa ni uhakiki wa idadi ya wapiga kura kwa kila kituo.

9.0 Mambo Muhimu ya Kuzingatiwa na Wapiga Kura na Wananchi
(a)    Sifa za Mpiga Kura
  • Mpiga kura ni raia yeyote wa Tanzania,
  • Aliyefikisha umri wa miaka 18,
  • Aliyeandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,
  • Mwenye kadi ya kupigia kura iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
  • Lazima awe Mkazi wa eneo analotaka kupiga kura na jina lake limeorodheshwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura au Orodha iliyobandikwa katika Kituo cha Kupigia Kura.
  • Orodha ya Wananchi wanaoshahili kupiga kura itabandikwa kwenye Vituo husika siku 8 kabla ya Uchaguzi hivyo wananchi wapitie Orodha hiyo mapema ili wajue vituo watakavyopigia kura.  
  • Vituo vyote vya kupigia kura havitawekwa katika nyumba za watu binafsi, vituo vidogo vya Polisi wala nyumba za Ibada kwa lengo la kuwapa nafasi na uhuru wapiga kura.
  • Katika zoezi la Kupiga Kura kipaumbele kitatolewa kwa watu wenye Ulemavu, Wanawake Wajawazito na wale wenye Watoto Wachanga, Wagonjwa na Wazee ili wasikae muda mrefu kwenye mistari.
  • Wapiga kura wasioweza kupiga kura wao wenyewe, wasioona au wasiojua kusoma watasaidiwa na watu watakao wateua wao wenyewe. Aidha, Tume imeandaa kifaa (Tactile Ballot Folder) kitakachowasaidia wapiga kura wasioona ili waweze kupiga kura zao wao wenyewe.
  • Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na vitafungwa saa 10.00 Jioni, iwapo kutakuwa na wapiga kura katika mistari muda huo, wapiga kura hao wataruhusiwa kupiga kura. Aidha, wapiga kura watakaofika baada ya muda huo hawataruhusiwa kupiga kura.
10.0 Makosa ya Uchaguzi (Makosa ya Jinai kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Sura 343 na Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Sura 292)
  • Kujaribu kupiga kura wakati muda wa kupiga kura umekwisha,
  • Kujaribu kupiga kura wakati hauruhusiwi kisheria kupiga kura,
  • Kujaribu kupiga kura zaidi ya mara katika uchaguzi,
  • Kujaribu kupiga kura kwa kutumia kadi ya mtu mwingine,
  • Kuweka kitu kingine zaidi ya karatasi ya kupigia kura katika sanduku la kuhifadhia kura.
  • Kuchana orodha ya wapiga kura au mabango yoyote ya elimu kwa mpiga kura.
  • Kughushi au kuharibu karatasi ya kura,
  • Kuchapisha na kusambaza karatasi za kura bila mamlaka kisheria,
  • Kupokea au kutoa rushwa kabla na wakati wa uchaguzi,
  • Kumzuia mtu kupiga kura yake kwa uhuru na amani,
  • Kutoa siri ya mpiga kura mwenzio kuwa anakwenda kumpigia kura Fulani au amempigia mtu Fulani.
  • Kuvaa au kuonesha alama yoyote ya chama wakati wa zoezi la upigaji kura.
  • Kuchukua kadi za Wapiga Kura ili wasiweze kupiga Kura.
  • Kutumia vitisho na nguvu kuwashawishi wapiga kura ili wakupigie kura.

11.0 Ulinzi na Usalama
Mkoa wa Iringa umejipanga vizuri kuhakikisha amani na usalama kwa kipindi chote cha kampeni za Uchaguzi na wakati wa zoezi la kupiga kura vyote vinafanyika vizuri kwa mujibu wa ratiba na kwa kuzingatia sheria za nchi ili Wananchi waendelee kuwa salama na kutekeleza majukumu yao.

Napenda kutoa rai kwa wananchi wote wa Mkoa wa Iringa kufahamu na kukubaliana kuwa yapo maisha na yataendelea kuwepo hata baada ya Uchaguzi Mkuu hapo tarehe 25 Oktoba, 2015. Hivyo, kila mmoja wetu lazima atimize wajibu wake katika kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kuwepo katika kipindi hiki chote ili tumalize zoezi hili tukiwa wamoja na wenye mshikamano mkubwa.

Katika kuhakikisha mkoa unakuwa na utulivu kwa kipindi chote, nimekutana na makundi mbalimbali kujadili suala la amani kuelekea Uchaguzi Mkuu. Makundi hayo ni viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa madhehebu ya dini, wazee na watu wenye ushawishi katika jamii na waandishi wa habari.
Lengo ni kupata maoni yao na ushauri wa jinsi ya kufanikisha Uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu.

Napenda kuchukua nafasi hii kuwathibitishia Wananchi wa Mkoa wa Irirnga kuwa, ulinzi utakuwepo wa kutosha katika kipindi chote cha kampeni na siku ya kupiga kura tarehe 25/10/2015.

Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kuwalinda wananchi wote, hivyo, rai yangu kwa Wananchi ni kuwa jitokezeni kwa wingi siku ya kupiga kura mapema na baada ya kupiga kura rudini kwenye maeneo yenu kuendelea na shughuli nyingine. Wananchi wasibaki kwenye vituo vya kupigia kura baada ya kupiga kura.
Asanteni kwa kunisikiliza

Wednesday, September 23, 2015

TASAF WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UWAZI NA UWAJIBIKAJI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kulipa uzito tatizo la utapiamlo ili kupunguza udumavu, ulemavu na vifo vya watoto na wanawake wanaonyonyesha.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua mkutano wa kamati za lishe za halmashauri na mkoa wa Iringa  kuhusu masuala ya lishe ya mama na mtoto katika ukumbi wa Veta.
Masenza alisema “matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata kuua watoto wetu na wanawake hasa wale wajawazito na wanaonyonyesha. Pia jamii kwa ujumla imekuwa ikiathirika kwa njia moja au nyingine kwa kuwepo kwa utapiamlo”. Masenza aliongeza “pamoja na maendeleo ambayo nchi yetu imeyapata katika maeneo mbalimbali, bado tatizo la lishe duni linaendelea kuathiri uchumi na kuchangia kuwepo kwa umasikini. Lishe duni pia huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili hivyo kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na taifa”.
Alisema kuwa uboreshaji wa hali ya lishe nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na kupunguza umasikini kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Aliongeza kuwa kwa upande wa watoto lishe husaidia kuongeza uwezo wao kiakili na usanisi shuleni.
Mkurugenzi wa Mwanzo bora Dkt. Daniel Nyagawa alilitaja lengo kuu la mradi huo kuwa ni kuisaidia serikali katika kutekeleza mkakati wa taifa wa lishe pamoja na mkakati wa taifa wa kubadili tabia na mienendo ya maisha.
Aliongeza kuwa mradi wa lishe wa mwanzo bora unalenga kupunguza upungufu wa damu kwa wajawazito na wanawake wanaonyonyesha kwa asilimia 20. Aidha, unalenga kupunguza udumavu kwa watoto chini ya umri wa miaka miwili kwa asilimia 20. Mwisho mradi unalenga kujengea uwezo wa utekelezaji kwa serikali mashirika yasiyo ya kiserikali na kijamii.
Dkt. Nyagawa alisema kuwa mradi unatumia mkakati wa mawasiliano yanayolenga kubadili tabia katika masuala ya lishe. Alisema kuwa mradi unalenga tabia ambazo zikifuatwa zitaleta matokeo makubwa katika kupunguza udumavu na upungufu wa damu. Aliongeza mradi unalenga kubadilisha tabia binafsi ambazo zamani miradi mingi haikufanya.
Akiongelea walengwa wa mradi huo, Dkt. Nyagawa aliwataja “walio ndani ya siku 1,000 tangu kutungwa kwa mimba hadi mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili”.Alifafanua kuwa ni mama mjamzito, anayenyonyesha na mama mwenye mtoto umri usiozidi miaka miwili. Baba ambaye mwenza au mke wake ana sifa zilizotangulia na wale wote wanaolea watoto wenye umri usiozidi miaka miwili.
Mradi wa lishe wa mwanzo bora ni mradi wa lishe uliofadhiliwa na serikali ya marekani kupitia USAID ukitekelezwa katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Dodoma, Manyara na Mbeya.
=30=                                          

JAMII YATAKIWA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kulipa uzito tatizo la utapiamlo ili kupunguza udumavu, ulemavu na vifo vya watoto na wanawake wanaonyonyesha.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua mkutano wa kamati za lishe za halmashauri na mkoa wa Iringa  kuhusu masuala ya lishe ya mama na mtoto katika ukumbi wa Veta.
Masenza alisema “matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata kuua watoto wetu na wanawake hasa wale wajawazito na wanaonyonyesha. Pia jamii kwa ujumla imekuwa ikiathirika kwa njia moja au nyingine kwa kuwepo kwa utapiamlo”. Masenza aliongeza “pamoja na maendeleo ambayo nchi yetu imeyapata katika maeneo mbalimbali, bado tatizo la lishe duni linaendelea kuathiri uchumi na kuchangia kuwepo kwa umasikini. Lishe duni pia huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili hivyo kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na taifa”.
Alisema kuwa uboreshaji wa hali ya lishe nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na kupunguza umasikini kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Aliongeza kuwa kwa upande wa watoto lishe husaidia kuongeza uwezo wao kiakili na usanisi shuleni.
Mkurugenzi wa Mwanzo bora Dkt. Daniel Nyagawa alilitaja lengo kuu la mradi huo kuwa ni kuisaidia serikali katika kutekeleza mkakati wa taifa wa lishe pamoja na mkakati wa taifa wa kubadili tabia na mienendo ya maisha.
Aliongeza kuwa mradi wa lishe wa mwanzo bora unalenga kupunguza upungufu wa damu kwa wajawazito na wanawake wanaonyonyesha kwa asilimia 20. Aidha, unalenga kupunguza udumavu kwa watoto chini ya umri wa miaka miwili kwa asilimia 20. Mwisho mradi unalenga kujengea uwezo wa utekelezaji kwa serikali mashirika yasiyo ya kiserikali na kijamii.
Dkt. Nyagawa alisema kuwa mradi unatumia mkakati wa mawasiliano yanayolenga kubadili tabia katika masuala ya lishe. Alisema kuwa mradi unalenga tabia ambazo zikifuatwa zitaleta matokeo makubwa katika kupunguza udumavu na upungufu wa damu. Aliongeza mradi unalenga kubadilisha tabia binafsi ambazo zamani miradi mingi haikufanya.
Akiongelea walengwa wa mradi huo, Dkt. Nyagawa aliwataja “walio ndani ya siku 1,000 tangu kutungwa kwa mimba hadi mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili”.Alifafanua kuwa ni mama mjamzito, anayenyonyesha na mama mwenye mtoto umri usiozidi miaka miwili. Baba ambaye mwenza au mke wake ana sifa zilizotangulia na wale wote wanaolea watoto wenye umri usiozidi miaka miwili.
Mradi wa lishe wa mwanzo bora ni mradi wa lishe uliofadhiliwa na serikali ya marekani kupitia USAID ukitekelezwa katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Dodoma, Manyara na Mbeya.
=30=                                          

WANAWAKE IRINGA WATAKIWA KUPIMA SARATANI YA KIZAZI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wanawake mkoani Iringa wametakiwa kujitokeza kupima saratani ya mlango wa kizazi ili wanapogundulika na saratani hiyo waanze matibabu mapema.
Wito huo umetolewa na mganga mkuu wa mkoa wa Iringa, Dkt. Robert Salim alipokuwa akifungua semina ya kufuatilia utekelezaji wa mipango na maazimio yaliyowekwa kuhusu kukabiliana na saratani ya mlango wa kizazi iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha afya ya msingi mjini Iringa.
Dkt. Salim alisema kuwa saratani ya mlango wa kizazi inasababisha maradhi na vifo kwa wanawake wengi nchini isipotambuliwa na kuanza kutibiwa mapema. Alisema kuwa wanawake wote walioanza mahusiano ya kimapenzi wanatakiwa kujitokeza katika vituo vya afya kupima ili wanapogundulika wameathirika na saratani hiyo waanze tiba mapema. Alisema kuwa yapo mahusiano makubwa baina ya maambukizi ya virusi vya ukimwi na saratani ya mlango wa kizazi. Kutokana na mahusiano hayo ambayo kwayo mkoa wa Iringa umeathirika sana na maambukizi ya ukimwi kwa 9.1% hivyo kusababisha ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi kuwa juu.
Nae Mkurugenzi wa uboreshaji afya kutoka taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Dkt. Sarah Maongezi alisema kuwa semina hiyo ililenga kufuatilia utekelezaji wa mipango na maazimio ya awali waliyojiwekea katika kukabiliana na tatizo la saratani ya mlango wa kizazi mkoani hapa. Alisema kwa kuwa mkoa wa Iringa ulianza muda mrefu mapambano dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi hivyo mkoa unatakiwa kuwa umepiga hatua za mafanikio zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine nchini. Alisema kuwa kwa hatua iliyofikiwa na mkoa wa Iringa, mkoa huo unaweza kujihamasisha kununua vifaa na vifaa tiba kwa lengo la kukabiliana na saratani ya mlango wa kizazi.
Saratani ya mlango wa kizazi ni miongoni mwa magonjwa yanayosababisha vifo kwa wanawake wengi ikikadiriwa kuwa zaidi ya wanawake 4,000 hupoteza maisha nchini kila mwaka.
=30=