Monday, August 26, 2013

Ag. RAS IRINGA ATAKA WADAU WOTE KUSHIRIKI KULINDA AMANI





Ushirikiano wa wananchi wote na wadau unahitajika katika kuhakikisha serikali inatimiza jukumu lake la kulinda na kusimamia amani na uslama nchini. 

          Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu

              Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi

           Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo


              Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evarista Kalalu
 
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu alipokuwa akichangia katika mkutano wa amani mkoa wa Iringa uliyoandaliwa na Jumuiya ya waislamu wa Ahmadiyya na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa. 

Wamoja amesema “serikali inalojukumu la kuhakikisha kuwa amani na usalama kwa watu wote, lakini katika kutekeleza hilo unahitajika ushirikiano wetu sote”. Amesema kuwa wananchi na wadau wote hawana budi kushirikiana katika kuhakikisha kuwa amani inadumishwa nchini. Amesema kuwa upendo ni nguzo mihumu katika kudumisha amani. Amesema amani haiwezi kuwepo kama hakuna upendo, na kushauri kuwa viongozi wote wajitahidi kuhubiri upendo ili kujihakikishia uendelevu wa amani.

Katika mchango wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi amesema kuwaamani haiwezi kutafsiriwa kwa tafsiri moja pekee, bali inatafsiriwa kwa sifa zake. Amezitaja sifa hizo kuwa ni ukosefu wa vurugu na migogoro. Sifa nyingine amezitaja kuwa ni pamoja na ukosefu wa vurugu na uadui. Nyingine ni ukosefu wa chuki na ugomvi. 

Mungi amesema kuwa amani ya kweli inazo tabia sinazoonekana. Amezitaja tabia hizo kuwa ni kujali, kuheshimu, haki kwa watu wengine. Amesema kuwa tabia nyingine ni ukarimu na uvumilivu kwa imani ya watu wengine.

Amesema kuwa amani haishikiki bali ipo katika akili na roho na inapimika kwa kutokuwepo kwa vurugu. 

Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo amesema kuwa amani ni kichocheo kikubwa cha maendeleo nchini. Amesema kuwa ili jamii iweze kuwa na maendeleo ni lazima watu na makundi yote waweze kutii mamlaka zilizopo kisheria kwa sababu mamlaka zote zinatoka kwa Mungu. 

Evarista Kalalu amewataka wadau wote wa amani kujiuliza wamefanya nini katika kuhakikisha amani iliyopo inadumu na kuwa endelevu. “Tanzania hatuna mahali pa kukimbilia iwapo tutaamua kuvunja amani iliyopo. Wote wasio na amani wanakimbilia kwetu, hivyo sisi tutakimbilia kwa nani?” alihoji Mkuu wa Wilaya ya Mufindi. 

Amesema kuwa ni ukweli usiofichika kuwa katika jamii tunayoishi wapo watu wasiopenda amani hivyo ni jukumu letu kuwaripoti katika mamlaka husika. “Si kila mtu anaweza kuchukua hatua, hivyo tunahitaji kuwalinda wale wote wenye mamlaka za kuchukua hatua” alisisitiza Evarista. 
=30=

No comments:

Post a Comment