Wednesday, January 31, 2018

USHIRIKIANO WA CHAMA NA SERIKALI WAPONGEZWA KILOLO



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Iringa
Kamati ya Bunge ya utawala na serikali za mitaa imepongeza ushirikiano baina ya serikali na chama tawala wilayani Kilolo kwa maendeleo ya wananchi.

Pongezi hizo zilitolewa na mjumbe wa kamati ya Bunge ya utawala na serikali za mitaa, Magreth Sitta katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Kilolo wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kilolo hivi karibuni.
 
Magreth Sitta, Mbunge wa Urambo
Sitta ambaye ni mbunge wa Urambo alisema kuwa mshikamano baina ya serikali na chama tawala ni muhimu katika kufanikisha dhamira ya serikali ya kuwaletea maendeleo wananchi. Alisema ili mchakato wa maendeleo uende vizuri ni muhimu kwa serikali na chama tawala kuzungumza lugha moja. Chama tawala kinawajibu wa kuisimamia serikali katika utekelezaji wa Ilani ya chama.
=30=

No comments:

Post a Comment