Wednesday, September 23, 2015

FOX APONGEZWA KWA KAZI ZA KIJAMII MUFINDI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza amepongeza kazi za kijamii zinazofanywa na muwekezaji Geoff Fox kwa lengo la kuwapunguzia umasikini wananchi wa Mufindi.
Pongezi hizo alizitoa alipotembelea shughuli za maendeleo zinazofanywa na muwekezaji huyo wilayani Mufindi kwa lengo la kujifunza pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa. “Nimefurahishwa na kazi za kijamii zinazofanywa na muwekezaji za kuisaidia jamii katika sekta za afya, elimu na ustawi wa jamii. Kazi hizi ni jukumu letu kama serikali lakini kutokana na sera yetu ya ushirikishaji jamii na sekta binafsi, sekta binafsi inapata fursa ya kusaidia juhudi hizi za kimaendeleo” alisema Masenza.
Alipotembelea zahanati ya Mdabulo inayomilikiwa na kanisa katoliki Jimbo la Iringa, mkuu wa mkoa alipongeza kazi nzuri inayoendelea kufanywa na zahanati hiyo iliyoanzishwa mwaka 1946 ikiwa umbali wa km 48 kutoka mjini Mafinga. Masenza alishauri uandaliwe utaratibu wa kutoa elimu ya magonjwa ya kisukari na saratani na mlango wa kizazi kutokana na magonjwa hayo kutokupewa kipaumbele. “Magonjwa ya kisukari na saratani ya mlango wa kikazi yamekuwa hayapewi umuhimu sana lakini yanachangia sana katika vifo vya wananchi wetu. Ni vizuri mkaweka utaratibu wa kuwa mnatoa elimu ya utambuzi na kujikinga na magonjwa haya ili kupunguza hatari ya vifo” alisema Masenza. Masenza aliiagiza halmashauri kununua mitungi …na siki ili kusaidia uchunguzi wa saratani hiyo.
Mkuu wa mkoa aliwaagiza wataalamu wa sekta ya afya wa halmashauri ya wilaya ya mufindi kuweka utaratibu wa kuitembelea zahanati ya Mdabulo mara kwa mara na kutoa ushauri wa kitaalam.
Kutokana na zahanati hiyo kuwahudumia wananchi wengi, mkuu wa mkoa alimuagiza mganga mkuu wa mkoa kufuatilia mchakato wa kuipandisha hadhi zahanati ya Mdabulo kuwa kituo cha afya ufanyike haraka…ili…
=30=
 

No comments:

Post a Comment