Thursday, January 18, 2018

MAAFISA UGANI WATAKIWA KITIMIZA WAJIBU KUHAMASISHA KILIMO CHA KOROSHO IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Maafisa ugani katika maeneo yanayolima zao la korosho wilayani Iringa wametakiwa kutimiza wajibu wao katika kukifanya kilimo cha korosho kuwa chenye tija.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akizindua kilimo cha zao la koroso katika kijiji cha Idodi wilayani Iringa jana.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliwataka maafisa ugani na viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya kijiji hadi tarafa wa maeneo yanayolima zao la korosho kutimiza wajibu wao katika kulifanya zao hilo kuwa na tija. 

Tunataka Mkoa ufanikiwe katika kilimo cha zao hili na ushauri wangu itungwe sheria ndogo itakayomlazimisha kila mkulima kushiriki katika kilimo hiki kinachotarajiwa pia kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya kubangua korosho,” alisema mkuu wa Mkoa.

Vilevile, aliwataka viongozi hao kuanzisha mashamba darasa yatakayotumika kihamasisha wananchi na kutumika kwa mafunzo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya alisema kuwa Halmashauri yake imezalisha miche 69,855 itakayotolewa bure kwa shule za msingi na sekondari na wananchi walio tayari kwa mashamba yao kupandwa. Alisema kuwa bodi ya korosho imedhamini upatikanaji wa miche hizo ili kuhamasisha zao hilo wilayani Iringa.

Masunya alisema kuwa katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huo shule za msingi zitapewa miche 3,672 itakayopandwa katika mashamba ya ekari 136. Aliongeza kuwa eneo la ekari 14 linalomilikiwa shule za sekondari litapandwa miche 378. Aliongeza kuwa wananchi watapewa miche 65,803 itakayopandwa katika eneo la ekari 2,437.

Vijiji vitakavyo zao la korosho linaweza kustawi ni Idodi, Mahuninga, Mlowa, Ilolompya, Mlenge, Itunundu, Kising’a, Kihorogota, Nyang’oro, Nzihi na Kiwele.
=30=

No comments:

Post a Comment