NA
|
TIMU
|
1
|
RAS IRINGA 1-0 IRUWASA
|
2
|
MAGEREZA 0-0 TANROADS
|
3
|
MKWAWA 4- 2 KLERUU
|
4
|
KIUMAKI 5-1 SIDO
|
5
|
DIRA 3-I IRUWASA
|
6
|
AIRPORT 3-0 POSTA
|
7
|
TRA 1-1 MAGEREZA
|
Sunday, January 28, 2018
MATOKEO YA MASHINDANO YA MPIRA WA MIGUU KWA TAASISI MKAONI IRINGA
Sunday, January 21, 2018
TIMU YA RAS IRINGA WAPOTEANA UWANJANI BAADA YA KICHAPO CHA 5-0 TOKA TANROADS
Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Timu
ya mpira wa miguu ya RAS Iringa imechapwa magoli 5-0 na wakala wa Barabara (TANROADS) katika mechi ya
ufunguzi iliyoshuhudiwa na mamia wa wakazi wa Manispaa ya Iringa wakiongozwa na
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela.
Mechi
hiyo iliyochezwa katika dimba la chuo cha Ualimu Kleruu kilichopo manispaa ya
Iringa ilianza kwa kasi ndogo huku kila timu ikosoma mchezo wa mwezake. Hadi
kipinci cha kwanza kinaisha timu ya RAS IRINGA ilikuwa nyuma kwa goli Moja. Kipindi
cha pili kilianza kwa kasi kidogo.
Jitihada za RAS IRINGA kurudisha goli
zilionekana wazi kabla ya juhudi hizo kufifishwa baada ya golikipa wao namba moja
Mashaka Mwanage kuumia mkono wa kuume na kushindwa kuendelea na mchezo. Pigo
hilo kwa RAS IRINGA lilifungulia mvua ya magoli hadi kufikia magoli matano.
Tangu
awali TANROADS walionekana kukamia mechi hiyo huku wakiwa na kikundi cha
washangiliaji mahili. Muda wote wa mchezo meneja wa TANROADS Mhandisi Daniel
Kindole alikuwa akifuatilia kwa makini mechi hiyo.
Baada
ya kipeng cha mwisho watumishi wa RAS walionekana kuondoka mmoja mmoja kwa njia
yake jambo lililotafsiriwa na wachambuzi wa masuala ya soka kuwa ni kuvurugwa
na kichapo hicho.
=30=
WATUMISHI WANAOSHIRIKI MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU MKOANI IRINGA WATAKIWA KUCHEZA KWA NIDHAMU
Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Watumishi
wa taasisi mbalimbali mkoani Iringa wametakiwa kucheza kwa nidhamu na kuepuka
ugomvi katika mashindano ya mpira wa miguu yanayoendelea mkoani Iringa.
Kauli
hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya
ufunguzi wa mchezo wa mpira wa miguu kwa taasisi za mkoa wa Iringa iliyosomwa
kwa niaba yake na mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela katika uwanja wa
chuo cha ualimu Kleruu kilichopo Manispaa ya Iringa jana.
Masenza
aliwataka wachezaji hao kucheza kwa nidhamu na kuepuka kuchochea ugovi. Alisema
kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni burudani na unajenga urafiki hivyo, mashindano
hayo yatumike kutoa burudani na kujenga urafiki miongoni mwa wanamichezo hao.
Aliongeza
kuwa mashindano hayo yatumike kujenga uzalendo kwa watumishi wa umma na
watumishi wa taasisi zisizo za kiserikali mkoani Iringa. Aidha, aliwataka
wanamichezo hao kutengeneza mtandao utakaowaunganisha kama wanamichezo na
watumishi wa taasisi mbalimbali.
Katika
salamu za afisa michezo Mkoa wa Iringa, Kenneth Komba kabla ya kumkaribisha
mgeni rasmi, alisema kuwa michezo hiyo ni wazo la mkuu wa Mkoa wa Iringa kutaka
kuwaunganisha watumishi wa taasisi za Mkoa wa Iringa kupitia mchezo wa mpira wa
miguu. Alisema kuwa hadi kufikia jana jumla ya taasisi 21 zilikuwa zimejitokeza
kushiriki mashindano hayo.
Wakati
huohuo, mechi ya ufunguzi, timu ya Timu ya RAS Iringa ilikubali kichapo cha
magoli 5 bila kutoka TANROADS.
Mashindano
ya mpira wa miguu kwa taasisi za Mkoa wa Iringa ni mashindanao ya kwanza ya
aina yake kufanyika mkoani hapa yakikabiliwa na changamoto ya udhanimi.
=30=
Thursday, January 18, 2018
MAAFISA UGANI WATAKIWA KITIMIZA WAJIBU KUHAMASISHA KILIMO CHA KOROSHO IRINGA
Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Maafisa ugani katika maeneo yanayolima zao la korosho wilayani
Iringa wametakiwa kutimiza wajibu wao katika kukifanya kilimo cha korosho kuwa
chenye tija.
Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza
alipokuwa akizindua kilimo cha zao la koroso katika kijiji cha Idodi wilayani
Iringa jana.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliwataka maafisa ugani na viongozi
wa serikali kuanzia ngazi ya kijiji hadi tarafa wa maeneo yanayolima zao la
korosho kutimiza wajibu wao katika kulifanya zao hilo kuwa na tija.
“Tunataka Mkoa ufanikiwe katika kilimo cha
zao hili na ushauri wangu itungwe sheria ndogo itakayomlazimisha kila mkulima
kushiriki katika kilimo hiki kinachotarajiwa pia kuchochea uanzishwaji wa
viwanda vya kubangua korosho,” alisema mkuu wa Mkoa.
Vilevile,
aliwataka viongozi hao kuanzisha mashamba darasa yatakayotumika kihamasisha
wananchi na kutumika kwa mafunzo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa,
Robert Masunya alisema kuwa Halmashauri yake imezalisha miche 69,855
itakayotolewa bure kwa shule za msingi na sekondari na wananchi walio tayari
kwa mashamba yao kupandwa. Alisema kuwa bodi ya korosho imedhamini upatikanaji
wa miche hizo ili kuhamasisha zao hilo wilayani Iringa.
Masunya alisema kuwa katika awamu ya kwanza ya
utekelezaji wa mpango huo shule za msingi zitapewa miche 3,672 itakayopandwa
katika mashamba ya ekari 136. Aliongeza kuwa eneo la ekari 14 linalomilikiwa
shule za sekondari litapandwa miche 378. Aliongeza kuwa wananchi watapewa miche
65,803 itakayopandwa katika eneo la ekari 2,437.
Vijiji
vitakavyo zao la korosho linaweza kustawi ni Idodi, Mahuninga, Mlowa,
Ilolompya, Mlenge, Itunundu, Kising’a, Kihorogota, Nyang’oro, Nzihi na Kiwele.
=30=
IRINGA WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA KULIMA ZAO LA KOROSHO
Na
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wananchi wilayani Iringa wametakiwa kuitumia vizuri
fursa ya kilimo cha zao la korosho ili kuweza kujiongezea kipato.
Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina
Masenza alipokuwa akizindua kilimo cha zao la korosho katika kijiji cha Idodi wilayani
Iringa jana.
Masenza aliwataka wananchi kutumia kilimo cha zao la
korosho kama fursa ya kuondokana na umasikini.
“Kuanzishwa kwa zao hili
wilayani Iringa ni fursa kubwa itakayousaidia Mkoa na watu wake kupambana na
umasikini na kuongeza mapato yake.” Alisema Masenza.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliwataka maafisa ugani na
viongozi wa vijiji, kata na tarafa zinazolima zao hilo kutimiza wajibu wao ili
kukifanya kilimo cha zao hicho kiwe chenye tija.
“Tunataka Mkoa ufanikiwe katika kilimo cha zao hili na ushauri wangu
itungwe sheria ndogo itakayomlazimisha kila mkulima kushiriki katika kilimo
hiki kinachotarajiwa pia kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya kubangua korosho,”
alisema mkuu wa Mkoa.
Aidha, aliwataka viongozi wa vijiji kuwa mfano waa kuigwa
katika kilimo cha korosho na uhamasishaji wake ili wananchi waweze kujifunza
kupitia mashamba hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema kuwa
kilimo cha korosho kitampatia mwananchi matokeo ya uhakika kwa sababu bei yake
ni nzuri. Alisema kuwa kwa taarifa za karibuni kilo moja ya korosho
zilizobanguliwa inauzwa hadi shilingi 4,000.
=30=
Subscribe to:
Posts (Atom)