Sunday, January 28, 2018

MATOKEO YA MASHINDANO YA MPIRA WA MIGUU KWA TAASISI MKAONI IRINGA




NA
TIMU
1
RAS IRINGA  1-0  IRUWASA
2
MAGEREZA  0-0  TANROADS
3
MKWAWA 4- 2 KLERUU
4
KIUMAKI 5-1 SIDO
5
DIRA  3-I  IRUWASA
6
AIRPORT  3-0  POSTA
7
TRA  1-1  MAGEREZA

Sunday, January 21, 2018

MATUKIO KATIKA PICHA UFUNGUZI MICHEZO YA TAASISI MKOA WA IRINGA

TIMU YA RAS IRINGA WAPOTEANA UWANJANI BAADA YA KICHAPO CHA 5-0 TOKA TANROADS



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  
Timu ya mpira wa miguu ya RAS Iringa imechapwa magoli 5-0 na  wakala wa Barabara (TANROADS) katika mechi ya ufunguzi iliyoshuhudiwa na mamia wa wakazi wa Manispaa ya Iringa wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela.

Mechi hiyo iliyochezwa katika dimba la chuo cha Ualimu Kleruu kilichopo manispaa ya Iringa ilianza kwa kasi ndogo huku kila timu ikosoma mchezo wa mwezake. Hadi kipinci cha kwanza kinaisha timu ya RAS IRINGA ilikuwa nyuma kwa goli Moja. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kidogo. 
 
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akisalimiana na Peter Nyakigera
Jitihada za RAS IRINGA kurudisha goli zilionekana wazi kabla ya juhudi hizo kufifishwa baada ya golikipa wao namba moja Mashaka Mwanage kuumia mkono wa kuume na kushindwa kuendelea na mchezo. Pigo hilo kwa RAS IRINGA lilifungulia mvua ya magoli hadi kufikia magoli matano.

Tangu awali TANROADS walionekana kukamia mechi hiyo huku wakiwa na kikundi cha washangiliaji mahili. Muda wote wa mchezo meneja wa TANROADS Mhandisi Daniel Kindole alikuwa akifuatilia kwa makini mechi hiyo.

Baada ya kipeng cha mwisho watumishi wa RAS walionekana kuondoka mmoja mmoja kwa njia yake jambo lililotafsiriwa na wachambuzi wa masuala ya soka kuwa ni kuvurugwa na kichapo hicho.
=30=

WATUMISHI WANAOSHIRIKI MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU MKOANI IRINGA WATAKIWA KUCHEZA KWA NIDHAMU



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Watumishi wa taasisi mbalimbali mkoani Iringa wametakiwa kucheza kwa nidhamu na kuepuka ugomvi katika mashindano ya mpira wa miguu yanayoendelea mkoani Iringa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya ufunguzi wa mchezo wa mpira wa miguu kwa taasisi za mkoa wa Iringa iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela katika uwanja wa chuo cha ualimu Kleruu kilichopo Manispaa ya Iringa jana.
 
Mkuu wa Wilaya y Iringa, Richard Kasesela
Masenza aliwataka wachezaji hao kucheza kwa nidhamu na kuepuka kuchochea ugovi. Alisema kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni burudani na unajenga urafiki hivyo, mashindano hayo yatumike kutoa burudani na kujenga urafiki miongoni mwa wanamichezo hao. 

Aliongeza kuwa mashindano hayo yatumike kujenga uzalendo kwa watumishi wa umma na watumishi wa taasisi zisizo za kiserikali mkoani Iringa. Aidha, aliwataka wanamichezo hao kutengeneza mtandao utakaowaunganisha kama wanamichezo na watumishi wa taasisi mbalimbali.

Katika salamu za afisa michezo Mkoa wa Iringa, Kenneth Komba kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, alisema kuwa michezo hiyo ni wazo la mkuu wa Mkoa wa Iringa kutaka kuwaunganisha watumishi wa taasisi za Mkoa wa Iringa kupitia mchezo wa mpira wa miguu. Alisema kuwa hadi kufikia jana jumla ya taasisi 21 zilikuwa zimejitokeza kushiriki mashindano hayo.

Wakati huohuo, mechi ya ufunguzi, timu ya Timu ya RAS Iringa ilikubali kichapo cha magoli 5 bila kutoka TANROADS.

Mashindano ya mpira wa miguu kwa taasisi za Mkoa wa Iringa ni mashindanao ya kwanza ya aina yake kufanyika mkoani hapa yakikabiliwa na changamoto ya udhanimi.
=30=

Thursday, January 18, 2018

MAAFISA UGANI WATAKIWA KITIMIZA WAJIBU KUHAMASISHA KILIMO CHA KOROSHO IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Maafisa ugani katika maeneo yanayolima zao la korosho wilayani Iringa wametakiwa kutimiza wajibu wao katika kukifanya kilimo cha korosho kuwa chenye tija.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akizindua kilimo cha zao la koroso katika kijiji cha Idodi wilayani Iringa jana.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliwataka maafisa ugani na viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya kijiji hadi tarafa wa maeneo yanayolima zao la korosho kutimiza wajibu wao katika kulifanya zao hilo kuwa na tija. 

Tunataka Mkoa ufanikiwe katika kilimo cha zao hili na ushauri wangu itungwe sheria ndogo itakayomlazimisha kila mkulima kushiriki katika kilimo hiki kinachotarajiwa pia kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya kubangua korosho,” alisema mkuu wa Mkoa.

Vilevile, aliwataka viongozi hao kuanzisha mashamba darasa yatakayotumika kihamasisha wananchi na kutumika kwa mafunzo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya alisema kuwa Halmashauri yake imezalisha miche 69,855 itakayotolewa bure kwa shule za msingi na sekondari na wananchi walio tayari kwa mashamba yao kupandwa. Alisema kuwa bodi ya korosho imedhamini upatikanaji wa miche hizo ili kuhamasisha zao hilo wilayani Iringa.

Masunya alisema kuwa katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huo shule za msingi zitapewa miche 3,672 itakayopandwa katika mashamba ya ekari 136. Aliongeza kuwa eneo la ekari 14 linalomilikiwa shule za sekondari litapandwa miche 378. Aliongeza kuwa wananchi watapewa miche 65,803 itakayopandwa katika eneo la ekari 2,437.

Vijiji vitakavyo zao la korosho linaweza kustawi ni Idodi, Mahuninga, Mlowa, Ilolompya, Mlenge, Itunundu, Kising’a, Kihorogota, Nyang’oro, Nzihi na Kiwele.
=30=

IRINGA WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA KULIMA ZAO LA KOROSHO



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wananchi wilayani Iringa wametakiwa kuitumia vizuri fursa ya kilimo cha zao la korosho ili kuweza kujiongezea kipato.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akizindua kilimo cha zao la korosho katika kijiji cha Idodi wilayani Iringa jana.

Masenza aliwataka wananchi kutumia kilimo cha zao la korosho kama fursa ya kuondokana na umasikini. 

“Kuanzishwa kwa zao hili wilayani Iringa ni fursa kubwa itakayousaidia Mkoa na watu wake kupambana na umasikini na kuongeza mapato yake.” Alisema Masenza.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa aliwataka maafisa ugani na viongozi wa vijiji, kata na tarafa zinazolima zao hilo kutimiza wajibu wao ili kukifanya kilimo cha zao hicho kiwe chenye tija. 

Tunataka Mkoa ufanikiwe katika kilimo cha zao hili na ushauri wangu itungwe sheria ndogo itakayomlazimisha kila mkulima kushiriki katika kilimo hiki kinachotarajiwa pia kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya kubangua korosho,” alisema mkuu wa Mkoa. 

Aidha, aliwataka viongozi wa vijiji kuwa mfano waa kuigwa katika kilimo cha korosho na uhamasishaji wake ili wananchi waweze kujifunza kupitia mashamba hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema kuwa kilimo cha korosho kitampatia mwananchi matokeo ya uhakika kwa sababu bei yake ni nzuri. Alisema kuwa kwa taarifa za karibuni kilo moja ya korosho zilizobanguliwa inauzwa hadi shilingi 4,000.
=30=