Saturday, December 16, 2017

MRADI WA USAID TULONGE AFYA WAPONGEZWA KWA KUTUMIA APROCHI YA ‘SBCC’



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
USAID Tulonge Afya wapongezwa kwa kuchagua kutumia mbinu za mabadiliko ya tabia kwa wanajamii (Social Behavior Change Communication approach) katika kufanikisha malengo ya mradi huo.

Pongezi hizo zilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipokuwa akifungua kikao cha kuutambulisha mradi wa USAID Tulonge Afya unaotekelezwa na shirika la FHI 360 kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Gentle Hills mjini Iringa jana.
 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu
Ayubu alisema kuwa mradi huo umechagua kutumia mbinu za mabadiliko ya tabia kwa wanajamii (SBCC). 

Nimefurahishwa sana kwa kutambua umuhimu wa mbinu hii mliyoichagua katika kuleta mabadiliko hasa pale inapotumika kwa ufasaha” alisema Ayubu. 

Aidha, alimtaka meneja mradi wa kanda kusimamia vizuri mradi huo ili mwisho wa utekelezaji mabadiliko chanya ya tabia za wananchi yaweze kuonekana.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa aliutaka mradi wa USAID Tulonge Afya kusaidia kuongeza kasi katika utekelezaji wa mkakati wa Mkoa wa kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi. 

Natambua pia mkakati wa Mkoa ni kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya UKIMWI, kuhakikisha wanaoishi na maambukizi ya VVU wanakuwa na ufuasi mzuri wa dawa, kupunguza vifo vya mama na mtoto, kupunguza maambukizi ya Malaria pamoja na kuongeza matumizi ya huduma za uzazi wa mpango” alisema Ayubu.
=30=

No comments:

Post a Comment