Saturday, September 10, 2011

Reaction of World Leaders 

"On September the eleventh, enemies of freedom committed an act of war against our country. Americans have known wars but for the past 136 years, they have been wars on foreign soil, except for one Sunday in 1941.  Americans have known the casualties of war but not at the center of a great city on a peaceful morning. Americans have known surprise attacks but never before on thousands of civilians. All of this was brought upon us in a single day and night fell on a different world, a world where freedom itself is under attack.... 
We are not deceived by their pretenses to piety. We have seen their kind before. They are the heirs of all the murderous ideologies of the 20th century. By sacrificing human life to serve their radical visions - by abandoning every value except the will to power - they follow in the path of fascism, and Nazism, and totalitarianism. And they will follow that path all the way, to where it ends: in history's unmarked grave of discarded lies.... The course of this conflict is not known, yet its outcome is certain. Freedom and fear, justice and cruelty, have always been at war, and we know that God is not neutral between them.  This is not, however, just America's fight. And what is at stake is not just America's freedom. This is the world's fight. This is civilization's fight. This is the fight of all who believe in progress and pluralism, tolerance and freedom....Great harm has been done to us. We have suffered great loss. And in our grief and anger we have found our mission and our moment. Freedom and fear are at war. The advance of human freedom - the great achievement of our time, and the great hope of every time - now depends on us. Our nation - this generation - will lift a dark threat of violence from our people and our future. We will rally the world to this cause, by our efforts and by our courage. We will not tire, we will not falter, and we will not fail... I will not forget this wound to our country, or those who inflicted it. I will not yield - I will not rest - I will not relent in waging this struggle for the freedom and security of the American people." -President George W. Bush


 " I was stricken by news and television pictures coming from the United States this morning. It is impossible
 to fully comprehend the evil that would have conjured up such a cowardly and depraved assault upon
 thousands of innocent people.  There can be no cause or grievance that could ever justify such unspeakable
 violence.  Indeed, such an attack is an assault not only on the targets but an offense against the freedom and
 rights of all civilized nations. "  - Prime Minister Jean Chrétien, Canada 
 "There can be no doubt that these attacks are deliberate acts of terrorism, carefully planned and coordinated
 and as such I condemn them utterly. Terrorism must be fought resolutely wherever it appears."  - United
 Nations Secretary-General Kofi Annan


 Queen Elizabeth II said she was watching developments in "growing disbelief and total shock."
 "this terrible tragedy.... the entire  international community should unite in the struggle against terrorism 
 this is a blatant challenge to humanity." - President Vladimir Putin, Russia
 "France is deeply upset to learn of the monstrous attacks that have just struck the United States....  In these
 terrible circumstances, all French people stand by the American people. We express our friendship and
 solidarity in this tragedy." - President Jacques Chirac, France
 "Our hearts are with you and we are ready to provide any assistance at any time....This is a war between good
 and evil and between humanity and the bloodthirsty."  -Prime Minister Ariel Sharon, Israel
 "It was with horror that I learned of the abominable terrorist attacks on the World Trade Center in New 
 York
and the Pentagon in Washington in which so many innocent people have lost their lives. My
 government staunchly condemns these acts of terrorism. The German people are at the side of the United 
 States of America
in this difficult hour. I wish to express my deep-felt condolences and complete solidarity 
 to you and  the American people. Our thoughts and prayers go out to the victims and their families." 
 -Chancellor Gerhard Schroeder, Germany
 "There have been the most terrible, shocking events taking place in the United States of America within the last couple of hours.... We can only imagine the terror and carnage there and the many, many innocent people who have lost their lives .... perpetrated by fanatics who are utterly indifferent to the sanctity of human life, and we, the democracies of this world, are going to have to come together to fight it and eradicate this evil completely from our world." -Prime Minister Tony Blair, United Kingdom 
 "An attack on one is an attack on all" -NATO Secretary-General Lord Robertson after the alliance's 19 
 ambassadors decided to invoke Article 5 of the NATO charter for the first time in the alliance's history.
"this outrageous and vicious act of violence against the United States is unforgivable." -Prime Minister
 Junichiro Koizumi, Japan
 "Irrespective of the conflict with America it is a human duty to show sympathy with the American people, 
 and be with them at these horrifying and awesome events which are bound to awaken human 
 conscience." - Moammar Gadhafi, Libyan Leader
 "We want from here to express our solidarity and our support to all the victims of these acts of terrorism
 and  their family members. We reiterate our complete, emphatic rejection of all forms of violence and all
 forms of terrorism." - President Vicente Fox, Mexico
 "I send my condolences, and  the condolences of the Palestinian people to American President Bush and
 his government and to the American people for this terrible act....We completely condemn this serious 
operation.... We were completely shocked.... It's unbelievable, unbelievable, unbelievable."  -Palestinian 
Authority President Yasser Arafat 
 "Egypt firmly and strongly condemns such attacks on civilians and soldiers that led to the deaths of a 
 large number of innocent victims." -President Hosni Mubarak, Egypt
 "I wish to express, on behalf of the Chinese Government and people, our deepest sympathy and solicitude
 to you and, through you, to the Government and people of the United States. I wish also to extend
 our condolences to the families of the victims. The Chinese Government has consistently condemned and 
 rejected all forms of terrorist violence." -President Jiang Zemin, China
  Mohammad Khatami, President of Iran, said he felt "deep regret and sympathy with the victims." and said
 "it is an international duty to try to undermine terrorism."
 "these monstrous criminals  have demonstrated a vile and brutal affront against humanity." -Prime Minister 
 Silvio Berlusconi, Italy
 "Cuba laments and expresses its profound sadness for the loss of so many innocent lives and expresses our
 absolute rejection of acts of terrorism, wherever they may come from."  -Foreign Minister Felipe Perez
 Roque, Cuba
 "I hurry to express to you and your fellow citizens my profound sorrow and my closeness in prayer for the
 nation at this dark and tragic moment." -Pope John Paul II, Vatican City
 "no doubt this is a result of injustice the U.S practices against the weak in the world." - Sheikh Ahmed Yassin, 
 Spiritual Leader of Hamas
 "It is premature to level allegations against a person who is not in a position to carry out such attacks,
  it was a well-organized plan and Osama has no such facilities."" -Mullah Abul Salam Zaeef,
  Taliban's Ambassador to Pakistan

 "And just as your beautiful skyscrapers were destroyed and caused your grief, beautiful buildings and 
 precious homes crumbled over their owners in Lebanon, Palestine, and Iraq by American weapons....
 Americans should feel the pain they have inflicted on other peoples of the world, so as when they suffer, they will find the right solution and the right path. " - President Saddam Hussein, Iraq
North Korea called the attacks "tragic," adding that it "is opposed to all forms of terrorism." 
 "No, we did not do this, and we are not with you." -Ayatollah Khamenei, Iranian Supreme Religious Leader
 "This place may be bombed, and we will be killed. We love death. The U.S. loves life. That is the big 
 difference between us." -Osama bin Laden, to a visiting reporter 26 Nov 2001.
source of news is www.worldstatesmen.org

Wednesday, September 7, 2011

SHEREHE YA HARUSI YA BW N BIBI. SAMWELI S. NYAGAWA

 Wenyewe sasa Bw n Bibi. Samweli S. Nyagawa wakiingia ukumbini

Keki ya uhakika shukrani kwa mpambaji 

Mama Harry...! Mama Harry...! Mama Harry...! 

Mwenyewe Neema G. Mwaipopo kama sio wa nchi hii vile!

Bw na Bibi. Jonas Kilima na mtoto wao wakiwa katika tabasamu ukumbini 

Mr n Mrs. Dr. E. Mpuya ambaye pia ni Mkuu wa Kazi wa Bw. Samwel Nyagawa 

Mama Chota na ujumbe wake katika ukumbi wa RUCO kushuhudia sherehe ya harusi ya Sam 


Familia ya Mama Mdemu ikiingia ukumbini 

Mr n Mrs. Prof. S. Nyagawa wakiingia ukumbi wa chuo cha RUCO katika sherehe ya harusi ya kijana wao wa mwisho Samwel Nyagawa 

Bibi. Modesta Kaweni na Bibi Kiula katika sherehe ya harusi ya Sam

Bibi. Kiula, Bibi. Ambrose na Bibi. Chambala wamejiachia katika sherehe ya Harusi ya kijana wao Samwel S. Nyagawa 

Mr n Mrs. Bahati F. Golyama wakijinafasi katika sherehe ya Harusi ya Bw n Bibi. Samwel S. Nyagawa
WAZAZI WASHAURIWA KUTOINGILIA NDOA ZA WATOTO WAO
Wazazi wametakiwa kutoingilia NDOA za watoto wao na kushauriwa kuwaacha wastarehe katika NDOA zao kwa sababu kuwaingilia watoto katika ndoa zao ni kinyume na mpango wa MUNGU na ni chanzo cha mafarakano katika NDOA.

Ushauri huo ulitolewa na Baba Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Iringa, Askofu Jonas Mkane katika nenolake lililotangulia ufungishaji wa NDOA TAKATIFU kati ya Samwel S. Nyagawa na Catherine W. Mdemu.
 Samwel S. Nyagawa akimvisha PETE YA NDOA TAKATIFU Catherine W. Mdemu

Askofu Mkane amesema kuwa baadhi ya NDOA zimekuwa zikivunjika kutokana na wazazi kuingilia ndoa za watoto wao na kusisitiza kuwa ni jambo la aibu kwa wazazi hao kuhusika katika kuharibu NDOA za watoto wao.

Amesema kwa kuwa Samwel ameamua kumuoa Catherine, tendo hilo maana yake ni Dunia mzima hakuna tena mwanamke anayeweza kuwa mke wa Samwel na kusisitiza kuwa NDOA ni utawala Mtakatifu.

Askofu Mkane amesema kuwa mwanzilishi wa Taasisi hiyo (NDOA) ni MUNGU mwenyewe pale Bustani ya Eden aliposema “si vema mtu huyu akawa peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufa-nana naye”.
Amesema kazi kubwa na msingi aliyonayo na anayowajibika kwayo Catherine kwa Samwel ni UTII wakati kwa Samwel yeye ni KUMPENDA Catherine na hayo ndiyo maisha ya NDOA.

Akiongelea changamoto katika NDOA amewataka maharusi hao kutotarajia mteremko katika maisha ha ohayo mapya na kusisitiza kwa mujibu wa maandiko yanavyosema “wanaume kaeni na wake zenu kwa akili…”.

Mwisho Baba Askofu amewashauri kuweka pamoja rasilimali zao na kupanga mipango yao ya kimaisha pamoja ili kufikia mafanikio ya pamoja haraka.

Katika muda wote wa ibada hiyo ya NDOA TAKATIFU maharusi hao walionekana wenye utulivu mkubwa mbele za MUNGU huku wakianikizwa na tabasamu na bashasha za haja wakati nyuso zao zikitawaliwa na furaha isiyo kifani na dim-pose zisizojificha. 
Ndoa hiyo ilifuatiwa na sherehe bab kubwa ya kuwapongeza iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha RUCO.
                                                                                                                       

NDOA YA SAMWEL S. NYAGAWA NA CATHERINE W. MDEMU ILIVYOACHA HISHORIA

Nae Catherine W. Mdemu akasaini cheti cha ndoa yake.  

Hapa Samwel S. Nyagawa anaondoa ule ubishi wa kama umeoa tuoneshe cheti cha ndoa kwa kusaini cheti cha ndoa yake huku Catherine akihakiki saini inayotelewa..sasa watu wanajiuliza kwani alishaiona saini ya Sam?? 

Catherine W. Mdemu nae akamvisha PETE ya Ndoa Samwel S. Nyagawa. Sasa hebu mwangalie Catherine hapa...!! 

 Wakati wa Samwel S. Nyagawa kumvisha PETE ya Ndoa Catherine W. Mdemu ukawadia na tendo hilo likafanyika kwa ustadi mkubwa yaani kama wanataniana vile!

Sikiliza maneno hayo ya maharusi  

Unaweza kudhani Sam anasinzia eeh! hata mie nilidhani hivyo

Huku akijiamini Samwel S. Nyagawa nae aliutamkia Umma kuwa anamuoa Catherine W. Mdemu

Ulifika wakati wa Catherine W. Mdemu kuutamkia Umma kuwa anakubali kuolewa na Samwel. S. Nyagawa 

Tabasamu la Samwel S. Nyagawa asikwambie mtu, hilo pozi la Catherine W. Mdemu usilihoji

Maharusi Samwel S. Nyagawa na Catherine W. Mdemu (katikati) wakiwa na wapambe wao (pembeni)

Baba Askofu Jonas Mkane akiongoza sala ya Misa ya Ndoa ya Bw. Samwel S. Nyagawa na Bi. Catherine W. Mdemu  

 Maharusi Samwel s. Nyagawa na Catherine W. Mdemu wakiwa kanisani 

Maharusi Samwel s. Nyagawa na Catherine W. Mdemu wakiingia katika nyumba ya Ibada 

Mama mzazi wa Samwel Nyagawa, Mama Prof. Nyagawa (kushoto) na mama ambaye jina lake halikujulikana kwa mara moja wakiwa kanisani 


Maharusi Samwel S. Nyagawa na Mpambe wake wakiingia Kanisani

Maharusi Samwel S. Nyagawa na mpambe wake wakiingia Kanisani

Friday, September 2, 2011


KARIBUNI KATIKA BLOG YA WANAFUNZI WOTE POPOTE TANZANIA (MATUKIO NA WANAVYUO)

Kwanza tunapenda kuwasalimu sana Ndugu walimu na wanafunzi na wadau wote mliopo popote nchini Tanzania na Duniani kwa ujumla, Kwa heshima na Taadhima tunapenda kuwatambukisha kwenu Blog mpya kabisa inayo kwenda kwa jina la MATUKIO NA WANAVYUO ambapo lengo kubwa ni kuwakutanisha wanavyuo wote Nchi nzima na kubadilishana mawazo pia kujua nini kinaendelea kila wakati kupitia mtandao huu, Hatuna mengi sana ya kuandika hapa kwa maana mtandao wenu unajieleza vizuri kabisa, pia mtandao huu ni wanavyuo wote waliopo vyuoni sasa na wale walio maliza pia ni wa watanzania wote kwa ujumla kwa maana kuna mambo yanayo wahusu na muhimu. Tunawaomba mpitie kila kona ya mtandao huu na kutoa maoni kama yapo nini kiongezwe ama kuboreshwa zaidi, Tunawakumbusha tena mtandao huu ni wako. sisi tunaongoza tuu kwa mawasiliano zaidi tutumie Barua pepe kupitia
( twanavyuo@live.com)
tunatanguliza  shukrani zetu pia atakae pata taarifa hii ampe na mwenzake
Asanteni sana.
Matukio na wanavyuo Crew

KUTEMBELEA MTANDAO HUU BOFYA HAPA
http://www.tzwanavyuo.blogspot.com/

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,
Dkt. Christine Ishengoma


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt. Christine G. Ishengoma (Pichani)ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma kufanya ukaguzi wa kina katika magari yote yanayotumika kusafirisha abiria katika wilaya zote.
Katika agizo hilo, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, amesisitiza juu ya umuhimu wa kuyachunguza, kuyakagua na kuyazuia magari yote yenye hitilafu za kiufundi yasifanye kazi ya kusafirisha abiria na mizigo.
Lengo la agizo hilo ni kudhibiti matukio ya ajali ambazo zinaweza kugharimu maisha ya wananchi pindi ajali zinapotokea. Hii inafuatia tukio la hivi karibuni ambapo gari la abiria linalofanya shughuli zake kati ya Mbinga na Mbamba-bay kupata ajali na kusababisha vifo vya watu sita na wengine kujeruhiwa. Ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Chunya ikiihusisha gari lenye namba T.270 BDG.
Katika ajali hiyo, gari hilo lilikuwa limepakia abiria na mizigo miongoni mwake yalikuwa mafuta ya Diesel na Petrol, hivyo baada ya ajali kutokea, mafuta yalishika moto na kusababisha vifo hivyo.
Ili kutekeleza agizo hilo, Jeshi la Polisi Mkoa litatakiwa kukagua na kuwazuia wenye magari ya abiria kubeba mizigo ya mafuta ya diesel/petrol katika magari yao, kudhibiti na kuzuia gari kubeba abiria wengi zaidi ya uwezo wake na mwisho kuyazuia magari yote yasiyo na sifa na vigezo vya kubeba abiria kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria ya usalama barabani.
Mwisho, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote waliopoteza ndugu zao kufuatia vifo hivyo na aidha, anawatakia pole na kuwafariji abiria wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo na amesisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote waliosababisha ajali hiyo kutokea.
Imetolewa na:
Revocatus A. Kassimba,
Afisa Habari,
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,
RUVUMA.


Wednesday, August 24, 2011

ZIARA YA MKE WA BALOZI WA MAREKANI MKOANI IRINGA KATIKA PICHA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (kushoto) akiagana na
Meneja wa Hospitali ya Aga Khan-Iringa, Bibi. Veronica James (kulia) nje ya Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa



Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma akibadilishana mawazo na Mke wa Balozi wa Marekani nchi Tanzania, Bibi. Jacquiline Lenhardf alipofika kumsalimia Kaimu Mkuu wa Mkoa Ofisi kwake

ZIARA YA MKE WA BALOZI WA MAREKANI MKOANI IRINGA KATIKA PICHA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (kushoto),
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka (kulia) na
Afisa USAID-Tanzania, Bibi. Ludovica Tarimo (katikati)
katika picha ya pamoja mj ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Friday, August 19, 2011

…WAHIMIZWA KULA VYAKULA VYA ASILI

Wananchi wa Nyanda za Juu Kusini wametakiwa kujenga utamaduni wa kula vyakula vya asili na kuachana na vyakula vya kisasa ili kujenga na kuboresha afya zao.

Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Sara Dumba (kulia) akila ugali wa mtama kwa mlenda na Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Georgina Bundala (kushoto) akipata kikombe cha uji wa mtama katika kutoa hamasa ya ulaji wa vyakula vya asili.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Sarah Dumba wakati akihamasisha ulaji wa vyakula vya asili katika maonesho ya Wakulima na Wafugaji katika viwanja vya Johm Mwakangale, Uyole Mbeya.
Dumba amesema “nawahamasisha wananchi wote kujenga utamaduni wa kula vyakula vya asili ili kujenga na kulinda afya zao”.

Amesema ulaji wa vyakula vya asili unamfanya mtu kuwa na  nguvu na afya njema inayomfanya aweze kukabiliana na changamoto za kimaisha za kila siku na kutokuwa legelege.

Akiongea nje ya banda la maonesho la Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, huku akiendelea kula ugali wa mtama kwa mlenda na simbilisi, Dumba amesema kuwa anajisikia furaha sana kwa sababu anapata “kitu roho inapenda” kwa sababu anapata mlo kamili.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Georgina Bundala katika uhamasishaji huo amesema viongozi wanawajibu wa kuwahamasisha wananchi wanaowaongoza kwa mifano katika yale wanayoyahubiri.

Huku nae akiwa anapata kikombe cha uji wa mtama ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa ubunifu huo wa kuleta vyakula vya asili kwa uhamasishaji na si maneno matupu.

Amesema wananchi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini hususani mkoa wa Iringa wajenge utamaduni wa kulima zao la mtama ili kukabiliana na ukame unaotokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
TANI MIL 1.4 ZAONGEZEKA MAZAO YA CHAKULA NA BIASHARA IRINGA
Mkoa wa Iringa umefanikiwa kuongeza kilimo cha mazao ya chakula na biashara hadi kufikia tani milioni 1.4 katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru.

Kaimu Katibu Tawala Msaidize, Sehemu ya Uchumi na Sekta za Uzalishaji, Shenal S. Nyoni akifafanua jambo

Akiwasilisha taarifa ya mafanikio ya kilimo katika miaka 50 ya Uhuru, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Uchumi na Sekta za Uzalishaji, Shenal Nyoni katika Iringa Day iliyofanyika katika ukumbi wa JKT ndani ya uwanja wa John Mwakangale Uyole, Mbeya yanapofanyika maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Nyoni amesema “katika miaka ya 60 mkoa ulikuwa ukizalisha tani laki 3.05 za mazao hayo na hadi kufikia mwaka 2011 mkoa umefanikiwa kizalisha tani milioni 1.4”.

Amesema katika sekta ya uvuvi mkoa una mabwawa 4,167 yanayozalisha tani 1,449 za Samaki na kuuingizia shilingi bilioni 4.3 kwa mwaka.
Nyoni amesema kuwa mkoa pia ulishiriki katika mashindano ya mifugo ya Afrika Mashariki na kuchukua nafasi ya kwanza. Katika mashindano hayo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ndiyo ilichukua ushindi huo.

Akiongelea sekta ya viwanda amesema mkoa una viwanda vya kusindika na kuyaongezea mazao thamani. Mkoa una viwanda vikubwa vinne, viwanda vya kati 53 na 66 ni viwanda vidogo na mashine 1,992 za kusaga nafaka.

Awali akitoa salamu zake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema kuwa mkoa wa Iringa umefanikiwa kuzalisha chakula cha kuutosheleza mkoa kwa sehemu kubwa na kuonesha masikito yake kwa baadhi ya sehemu zinazokabiliwa na upungufu wa chakula kutokana na upungufu mkubwa na ukame ulioyakabili baadhi ya maeneo hayo.

Amesema mkoa umalima mazao mengi yakimo mazao ya biashara kama mbao, chai, pareto, kahawa, alizeti na maua.

SUMBAWANGA YAPUNGUZA VIFO VYA AKINA MAMA

Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imefanikiwa kupunguza idadi ya vifo vya akina mama hadi kufikia vifo 245 kati ya vizazi 100,000 mwaka 2010.

Hayo yamesemwa na Afisa Muuguzi wa Manispaa hiyo, A. Ngojo wakati akifafanua lengo namba mbili la Manispaa ya Sumbawanga la kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na ujauzito katika maonesho ya nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole- Mbeya.

Ngojo amesema kuwa hadi kufikia Disemba 2010 Manispaa ya Sumbawanga iliweza kufikia lengo kwa kupunguza vifo hiyo toka vifo 263 kati ya vizazi 100,000 mwaka 2008 hadi kufikia vifo 245 kati ya vizazi 100,000 Disemba, 2010.

Amezitaja hatua zilizofikiwa kuwa ni kutoa motisha kwa wakunga wa jadi wanaowapeleka wajawazito kujifungua kwenye vituo vya afya na kupata huduma za kitaalamu. Hatua nyingine ameitaja kuwa ni kuongeza watumishi wenye ujuzi kwenye vituo vya huduma za afya toka 61% kwa mwaka 2008 hadi 91% kwa mwaka 2010.

Vilevile, kuongeza huduma za mkoba za uzazi wa mpango kutoka vituo 7 kati ya 15 (47%) kwa mwaka 2008 hadi kufikia vituo 11 (73%). Pia kuihamasisha jamii kuhusu uzazi wa mpango na kuimarisha huduma za vifaa ikiwa ni pamoja na magari ya kubeba wagonjwa.

Aidha, Manispaa hiyo imefanikiwa kupunguza vifo vya watoto wa umri chini ya mwaka mmoja kutoka 37 kati ya watoto 1000 mwaka 2008 hadi 17 kati ya watoto 1000 kufikia Disemba 2010.


Wednesday, July 27, 2011

WATUMISHI WA RAS IRINGA WAPEWA SOMO LA RUSHWA 

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa ilianzisha Mkakati wa kudhibiti Rushwa mahali pa kazi ili Ofisi hiyo iwe ni eneo salama kutolea huduma kwa wananchi.
Paulos Lekamoi, Mwanasheria wa Sekretarieti ya Mkoa wa Iringa


Hayo yamesemwa na Mwanansheria wa Ofisi hiyo, Paulos Lekamoi wakati akiwasilisha mada juu ya Sheria ya Rushwa na Wajibu wa Watumishi wa Umma katika kudhibiti vitendo vya rushwa katika ukumbi wa Chuo kikuu Huria Tanzania tawi la Iringa katika Manispaa ya Iringa.

Lekamoi amesema “katika kuhakikisha rushwa mahali pa kazi haina nafasi ilianzisha mkakati wa kudhibiti rushwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa”.

Amesema mkakati huo umezingatia mkakati wa kitaifa wa kudhibiti rushwa ambapo lengo kuu ni kuimarisha njia za kupambana na rushwa, kuweka mifumo ya uadilifu, uwajibikaji na uwazi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na uzingatiaji wa Sheria ya Rushwa ya mwaka 2007.

Lekamoi amesema katika sehemu ya III ya Sheria Na. 11 imeleta mabadiliko makubwa sana yanayoenda sambamba na Azimio la Umoja wa Mataifa la Mwaka 2005. Amesema Sheria hii imeongeza makosa yaliyopo kwenye Sura ya 329 ya Sheria kama ilivyorekebishwa Mwaka 2000 na kuyataja baadhi ya makosa kuwa ni mchakato wa rushwa (kifungu cha 4), kutumia nyaraka mbalimbali kumpotosha msimamizi (kifungu cha 6), Maafisa wa Serikali kutumia madaraka yao kujinufaisha (kifungu cha 7), kupatikana na mali yoyote ambayo imepatikana kwa njia ya Rushwa (kifungu cha 10).

Amesema kifungu cha 15 (i) (a) na (b) cha Sheria Na. 11, 2007 kinazungunzia makosa yanayohusu upokeaji wa rushwa ambapo Mtumishi wa Umma anaweza kujikuta amejiingiza aidha kwa kujua au kwa kutojua.

Ameyataja makosa hayo kuwa ni kushirikiana na mtu mwingine au mtumishi mwenyewe kushawishi kupokea au kukubalikupokea chochote kwa manufaa yake ili kutekeleza lengo lolote ambalo kimsingi anatakiwa alifanye katika shughuli zake za kila siku.

Vilevile, kifungu Na. 15 (a) kinamtia hatiani mtu yeyote atakaetoa ahadi ya kumpendelea mtu yeyote.


Zaidi ya asilimia 70 ya matumizi ya kawaida ya Serikali ni kwa ununuzi wa bidhaa, huduma na malipo kwa kazi za ujenzi wa miundombinu.

Akiwasilisha mada juu ya Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2004, Uwezo wa Bajeti katika kufanikisha Manunuzi na Udhibiti wa Rushwa katika Manunuzi, Afisa Ugavi Msaidizi Mkoa wa Iringa, Janeth Kitinye amesema kuwa eneo la Manunuzi ya Umma ni muhimu sana kwa sababu hutumia sehemu kubwa ya fedha za walipa kodi wa Tanzania.

Bi. Janeth Kitinye, Afisa Ugavi Msaidizi Sekretarieti ya Mkoa wa Iringa akiwasilisha mada

Aidha, ufanisi katika eneo hili ni chachu ya kufikia baadhi ya malengo makubwa ya kiuchumi na kijamii ya Taifa.

Amesema kuwa ukiondoa mishahara ya watumishi wa Serikali, karibu asilimia 70 ya Matumizi ya kawaida ya Serikali ni Ununuzi wa bidhaa, huduma na malipo kwa kazi mbalimbali. Vilevile, amesema karibu asilimia 100 ya matumizi ya Maendeleo ni kwa ajili ya ununuzi wa bidhaa, huduma na malipo kwa ajili ya kazi za ujenzi wa miudombinu na miradi mingine ya Maendeleo.

Amewataka watumishi wa Umma kuona kuwa wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha Manunuzi wanayoyafanya yanawawezesha kupata bidhaa na huduma zenye Ubora kulingana na thamani ya fedha zilizotumika.

Kitinye amesema Sheria ya Manunuzi ya Umma ya Mwaka 2004, na Kanuni zake za Mwaka 2005 kwa pamoja zinaweka misingi na taratibu za kweza kufikia adhima hiyo.

Ameongoza kuwa Vitengo vya Manunuzi Vinajukumu la msingi la kuhakikisha kuwa huduma muhimu zinawafikia watumishi wa Umma na Wahitaji wengine katika muda uliopangwa na katika ubora unaokubalika. Sharia ya Manunuzi ya Mwaka 2004 na Kanuni zake za Mwaka 2005 zinawapngoza Watumishi wa Umma katika misingi ya Utawala Bora na uwajibikaji kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Thursday, June 9, 2011

MKOA WA IRINGA WAIBUKA MSHINDI WA USAFI NA MAZINGIRA

Mkoa wa Iringa umepongezwa kwa kuibuka mshindi wa jumla katika mashindno ya afya na usafi wa mazingira nchini na kupata zawadi ya kombe na kutakiwa mikoa mingine kuiga mfano huo ili mikoa yote iwe na mazingira safi na salama.
Hayo yamesemwa na mgeni rasmi, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Mizengo Pinda katika utoaji zawadi kwa washindi wa shindano la afya na usafi wa mazingira, aliyewakilishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka  kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyofanyika mjini Songea.
Katika mashindano hayo ya afya na usafi wa mazingira yaliyoratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Halmashauri za Manispaa (Iringa), Mji (Njombe) na Wilaya (Njombe) zimekuwa mshindi wa tatu (Manispaa ya Iringa), wa pili (Mji Njombe), na wa kwanza (Wilaya ya Njombe) katika ngazi ya Halmashauri za Manispaa, Miji na Wilaya.
Kitaifa Halmashauri ya Jiji la Mwanza ndiyo mshindi kati ya majiji matatu yaliyoshindanishwa. Kwa upande wa Halmashauri za Manispaa jumla ya Manispaa 17 zilishindanishwa na Manispaa ya Moshi iliibuka msindi ikifuatiwa na Arusha na Iringa. Upande wa Halmashauri za Miji jumla ya Halmashauri sita zilishindanishwa na Mpanda iliibuka mshindi ikifuatiwa na Njombe. Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ilizishinda Halmashauri za Meru (namba mbili) na Rungwe (namba tatu). 
Mkoa wa Iringa umeibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira baada ya Halmashauri zake tatu za Iringa, Mji Njombe na Wilaya ya Njombe kushinda katika nafasi tofauti.
Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa kitaifa kila mwaka tarehe 5 Juni na mwaka huu yameongozwa na kaulimbiu isemayo ‘panda miti na kuitunza: hifadhi mazingira’ mkoani Ruvuma katika Manispaa ya Songea. Maadhimisho haya kimataifa yamefanyika katika miji ya Delhi na Mumbai nchini India.