Thursday, June 9, 2011

JENGENI UTAMADUNI WA KUPANDA MITI
Watanzania wametakiwa kuachana na utamaduni wa kupanda miti kwa mazoea hasa katika kipindi cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira kitaifa na kujenga utamaduni kwa kupanda miti mara kwa mara ili kujihakikishia mazingira salama ya kuishi.
Rai hiyo imetolewa na Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka katika hotuba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda alipomuwakilisha kwenye kilele cha Maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani yaliyofanyika kitaifa katika Mkoa wa Ruvuma, manispaa ya Songea.
Prof. Tibaijuka amesema “kupanda miti si fasheni bali ni kazi ya kudumu” hivyo utamaduni wa kupanda miti katika siku za maadhimisho hauna budi kuachwa na kufanya upandaji miti kuwa ni zoezi endelevu.  Amesema mazingira ni sehemu ya maisha ya binadamu na uhai hivyo utunzaji wake ni jambo la lazima kwa kizazi hiki ili kijacho kiweze kujivunia hazina hiyo.
Amesema maadhimisho haya yanaongozwa na kaulimbiu isemayo ‘panda miti na kuitunza ili kuhifadhi mazingira’. Kaulimbiu inawataka watanzania kukaa chini na kutafakari na kujipima kama hatua zinazostahili zimechukuliwa katika kulinda.
Aidha, amesema kuwa misitu husaidia sana upatikanaji wa mvua jambo linalotegemewa sana katika kilimo na shughuli nyingine za kijamii. Vilevile, amekemea tabia inayoendelea kukua ya utakaji miti na uchomaji wa mioto ovyo. Amesema “kupanda miti si kuboresha mazingira tu bali na kuongeza kipato tukokana na mazao ya misitu”.
Awali katika utangulizi wake, Dkt.  Terezya  Huvisa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira amesema kuwa Serikali kupitia Wizara yake imeandaa mkakati wa kuhifadhi mazingira uliojikita katika kuielimisha na kuihamasisha jamii juu ya umuhimu wa mazingira na uhifadhi wa uoto wa asili.
Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ni matokeo ya azimio la umoja wa Mataifa la mwaka 1972, la Stockhorm –Sweden na kitaifa yalizinduliwa tarehe 1 Juni, 2011 katika kiwanja cha Majimaji kilichopo Manispaa na Makamu wa Rais, Dkt. Mohamed Gharib Bilal. Maadhimisho yaha yamekwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuri wa Tanzania na miaka 47 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


BAJETI YAUJENZI WA VIWANJA VYA MICHEZO IRINGA

Halmashauri za Mkoa wa Iringa zimeshauriwa kutenga bajeti ya kutosha ya kuhudumia michezo hasa ujenzi wa viwanja vya michezo ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa viwanja hivyo.
Ushauri huo umetolewa na George Lukindo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Njombe, wakati akifungua rasmi mashindano ya Umoja wa Michezo na Sanaa Sekondari Tanzania (UMISSETA) ngazi ya Mkoa yatakayopelekea kuundwa kwa timu ya UMISSETA ya Mkoa wa Iringa.
Lukindo amesema “upungufu wa viwanja vya michezo ni tatizo katika Mkoa wa Iringa kutokana na jiografia ya Mkoa wenyewe kutokuwa na maeneo mengi tambalale hivyo nazishauri Halmashauri za Mkoa huu zipange bajeti ya kutosha kwa shule kadhaa ili kujenga viwanja vya michezo”. Amesema huwezi kuongelea kuinua sekta ya michezo katika ngazi yoyote kama hutakuwa na viwanja vya kutosha na vilivyo katika ubora unaostahili kwa michezo husika.
Akiongelea ufinyu wa bajeti ya michezo ya UMISSETA, Lukindo amezishauri Halmashauri kuangalia uwezekano wa kuongeza fedha za ziada ili kufidia upungufu unaojitokeza.
Akisisitiza suala la nidhamu amesema mchezaji asiye na nidhamu UMISSETA si mahali pake. Amesema “mchezaji asiye na nidhamu hata kama atakuwa ni mzuri kiasi gani asiingizwe katika timu ya Mkoa”.
Wakati akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mashindano ya UMISSETA, Mwenyekiti wa UMISSETA Mkoa wa Iringa ambae pia ni Afisa Elimu Mkoa, Joseph Mnyikambi amesema kuwa michezo ni upendo, furaha na msikamano na kusisitiza kuwa katika kipindi chote cha mashindano hayo suala la nidhamu lipewe umuhimu wa pekee. Vilevile, amewaasa wanamichezo kuwa wanapokuwa uwanjani lazima watarajie na kukubali kushinda, kutoka sare au kushindwa.
Katika risala iliyoandaliwa na UMISSETA Mkoa na kusomwa na Upendo Mdzovela iliainisha changamoto zinazoikabili michezo ya UMISSETA kuwa ni pamoja ufinyu wa bajeti inayotengwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Aidha, changamoto nyingine ni upungufu wa walimu wenye taaluma ya michezo na vifaa vya michezo na upungufu wa viwanja vya michezo.
Mechi za ufunguzi zilizofana sana kwa kuzishindanisha timu za mpira wa miguu ya Halmashauri ya Mji Njombe wasiosikia (viziwi) na timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ambapo Ludewa waliibuka kidedea kwa ushindi wa 1-0. Katika mechi nyingine ya mpira wa pete timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa iliibwaga timu ya Wasiosikia ya Halmashauri ya Mji Njombe kwa mabao 7-3.
MAAFISA MICHEZO LAZIMA MUONEKANE

Maafisa Michezo wa Halmashauri wametakiwa kutoka na kushiriki katika shughuli zote za michezo katika Halmashauri zao ili kudhihirisha uwepo wao na kuinua kiwango cha michezo katika Mkoa wa Iringa.
Agizo hilo limetolewa na Kenneth Komba, Afisa Michezo Mkoa wa Iringa, wakati akizungumza katika kikao maalumu cha kuweka mikakati ya kufanikisha michezo ya Umoja wa Michezo na Sanaa Sekondari (UMISSETA) mkoani hapa kilichowakutanisha Wakuu wa Shule za Sekondari, Maafisa Elimu Taaluma Sekondari, Walimu wa Michezo na Afisa Michezo Mkoa muda mfupi baada ya kuzipokea timu za michezo mbalimbali ya UMISSETA kutoka katika Halmashauri nane za Mkoa wa Iringa uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari ya Mpeche Wilayani Njombe.  
Komba amesema ili kuimarisha michezo yote katika Mkoa wa Iringa “ni lazima Maafisa Michezo wa Halmashauri watoke na kushiriki katika shughuli za michezo katika Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wengine wa michezo kwa sababu nyie ndio wataalamu katika tasmia ya michezo”. Aidha, amesisitiza ushirikishwaji wa Maafisa Michezo hao katika shughuli za michezo ili jamii iweze kunufaika na taaluma yao.
Komba ambaye pia ni Meneja wa timu ya UMISSETA ya Mkoa aliushukuru uongozi wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) ngazi ya Wilaya na Mkoa kwa kujipanga na kufanikisha kuanza kwa mashindano ya UMISSETA mkoani hapa. Amesema kuwa TAHOSSA wamefanikisha kuanza kwa mashindano hayo kutokana na nguvu waliyonayo iliyojengeka katika misingi madhubuti ya umoja wao na kuheshimiana. Amesema jambo lolote la kimichezo haliwezi kukwama kwa namna yoyote ile hasa likiwa ni shirikishi kwa wadau na likifanyika kwa moyo wa umoja na mshikamano mkubwa.
Mwenyekiti wa TAHOSSA Mkoa wa Iringa, Andrew Kauta, amewataka walimu wote kusimamia kwa dhati suala la nidhamu kwa wanamichezo wote pasipo kujali mipaka ya Halmashauri au Wilaya zao na kusisitiza kuwa katika nidhamu hakuna mipaka. Aidha, amesisitiza kuwa michezo ni umoja, mshikamano na burudani hasa suala la nidhamu likidhibitiwa zaidi katika mavazi na matumizi ya lugha.
Vilevile, amewata walimu wa michezo kuwasilisha takwimu sahihi za wanamichezo na michezo wanayoshiriki kwa kila Halmashauri ili kuondokana na upotoshaji wa takwimu na usalama wa wanamichezo.
Lengo la msingi la mashindano haya ya UMISSETA ngazi ya Mkoa ni kushindanisha Wilaya sita na Halmashauri zake nane za Mkoa wa Iringa na hatimaye kupata timu moja ya Mkoa itakayokwenda kushiriki mashindano ya Kanda yanayotarajia kutimua vumbi Mkoani Ruvuma kuanzia tarehe 2 Juni, 2011.
Michezo ya UMISSETA inatarajia kuanza leo ngazi ya Mkoa katika Wilaya ya Njombe na inatarajia kushirikisha jumla ya wanamichezo 1088 katika michezo mbalimbali. 
KILIMO CHA MTAMA KIIMARISHWE

Viongozi wa Mkoa wa Iringa wameshauriwa kuweka juhudi za dhati katika kilimo cha mtama ili kukabiliana na baa la njaa linayoyakabili baadhi ya maeneo katika Wilaya za Iringa na Kilolo mkoani hapa.
Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Darry Rwegasira wakati akitoa uzoefu wa jinsi Wilaya ya Mpwapwa ilivyofanikiwa katika kilimo cha mtama na kukabiliana na baa la njaa.
Rwegasira amesema mapokeo ya viongozi ni jambo la msingi sana katika kufanikisha kilomo cha zao la mtama. Kwa upande wa Wilaya yake amesema “mapokeo ya viongozi wa Wilaya ya Mpwapwa ni mazuri sana”. Amesema Wilayani kwake kuanzia Mkuu wa Wilaya, Madiwani, Afisa Kilimo, Katibu wa CCM na Maafisa Watendaji wanalima zao la mtama jambo linalowafanya wananchi kuona mfano na umuhimu wa kilimo hicho kutoka kwa viongozi wao.
Mkuu wa Wilaya amesema kuwa Wilaya ilitengeneza sheria mdogondogo zinazosimamia utekelezaji wa mkakati wa kilimo cha mtama Wilayani hapo. Aidha, alishauri kuwa nguvu kupindukia zisitumike badala yake uhamasishaji na elimu ndio msingi pekee wa kuwafanya wananchi kukubaliana na kilimo hicho na kwa kuangalia mifano kutoka kwa viongozi wao.
Vilevile, mkakati mwingine uliotumika ulikuwa ni uundaji wa timu na kamati kuanzia ngazi za kijiji hadi Wilaya zikiwahusisha wataalamu wa kilimo na viongozi.
Wilaya ya Mpwapwa ilichagua kata tisa za mfano na kila kijiji kilikuwa na wakulima 98 wanaotumika kama walimu wa kuwaelimisha wenzao.
Nae kiongozi wa timu iliyokwenda kujifunza kilimo cha mtama Wilayani Mpwapwa, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Asseri Msangi, amewashauri wakulima wa Wilaya ya Mpwapwa kutumza ardhi vizuri dhidi ya uharibifu unaotokana na mmea uitwao kidua. Amesema kutokana na hatari yam mea huo kwa ardhi na mazao Serikali ya kikoloni ilitunga Sheria ya 1946 kwa ajili ya kulinda ardhi dhidi ya kuharibika. Msangi amesema “tunzeni ardhi yenu vizuri, ardhi ni mali msipoitunza mtaumbuka”, “msipoitunza ikaharibika mtaenda wapi kwingine tumejaa”. Vilevile, amewashauri wataalamu wa kilimo kuwa watu wanaopenda mabadiliko na kwenda na wakati katika kuboresha na kuinua kilimo. 
VYUO VIONGEZA MAPATO KWA KUANZISHA MIRADI

Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vimetakiwa kufikiria mikakati ya kuongeza mapato kwa kupitia miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujielekeza katika mahitaji ya msingi ya jamii inayovizunguka.
Rai hiyo imetolewa na Ummy Ally Mwalimu, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto alipotembelea chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Ruaha kilichopo katika Manispaa ya Iringa.
Mwalimu amesema “lazima mfikirie jinsi ya kuongeza mapato kwa kupitia miradi mbalimbali na mahitaji ya jamii ili muweze kuongeza mapato ya chuo”. Amesema vyuo vikiweka mkakati wa kuongeza mapato vitaweza kutatua matatizo yaliyo ndani ya uwezo wa vyuo husika badala ya kuisubiri Serikali kufanya kila kitu. Aidha, amevishauri vyuo vya maendeleo ya wananchi kuangalia fursa na vikwazo vilivyopo katika jamii na kuandaa programu za kuisaidia jamii. Ametolea mfano kuazisha programu za kuwawezesha kinamama kuondokana na umasikini na kujitegemea na programu za elimu ya ujasiliamali.
Naibu Waziri amehimiza kuendeleza na kudumisha ushirikiano baina Mkoa, Halmashauri na vyuo hivyo ili jamii iweze kunufaika na huduma zitolewazo kwasababu wote wanategemeana.
Awali alitembelea shule ya sekondari wasichana ya Iringa na kuongea na wasichana kwa minajili ya kuhamasisha maendeleo na usawa wa kijinsia na kuwatia moyo wanafunzi hao.
Kaimu Mkuu wa chuo cha maendeleo ya jamii Ruaha, Gaspar J. Msigala alizitaja baadhi ya changamoto zinazokikabili chuo hicho kuwa ni pamoja na upungufu wa miundombinu ya kitaaluma jambo linalosababisha udahili wa wanafunzi wachache ukilinganisha na uhitaji wa wanafunzi wanaotuma maombi na kuwa na sifa. Aidha, mkakati wa awali uliotumika kukabiliana na changamoto hiyo ni pamoja na kugawa wanafunzi katika awamu mbili za masomo yaani wanaoanzi asubuhi na wengine jioni.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto yupo katika ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani hapa kutembelea vyuo maendeleo ya jamii na vyuo vya maendeleo ya wananchi kuzifunza fursa na changamoto zilizopo, kuongea na watumishi na kuongeza hamasa ya kimaendeleo.
Chuo cha maendeleo ya jamii Ruaha kipo kilometa tatu kutoka Iringa mjini na kilianza mwaka 2007 baada ya kubadilishwa toka chuo cha maendeleo ya wananchi.    
MGAWANYO WA RASILIMALI USIO HAKI CHANZO CHA KUVUNJIKA KWA AMANI NCHINI

Mgawanyo wa rasilimali za nchi usio usiozingatia usawa na haki ni miongoni mwa vyanzo vya kuvunjika kwa amani katika jamii.
Rai hiyo imetolewa na Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Fredrick Sumaye katika hotuba yake wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo cha teknolojia ya Habari na mawasiliano (Orphanage ICT and School) kwa ajili ya watoto yatima mkoani Iringa iliyofanyika katika uwanja wa Samora mjini hapa.
Sumaye amesema “mgawanyiko wa mali usiozingatia usawa na haki na hasa utajiri unapojikusanya kwa wachache lazima amani itatoweka”. Amesema nchi ikiwa na matajiri sana na masikini wa kutisha hasa wakiwa ndio wezi sana amani hutoweka. Aidha, amesisitiza kuwa amani ni rasilimali kubwa kuliko zote katika taifa na pindi inapotoweka si rahisi kuirudisha.
Amesema kuwa ubaguzi na chokochoko za kiimani nazo huchangia uvunjifu wa amani. Amesisitiza kuwa “ubaguzi wa dini unapoota mizizi amani huyeyuka kama pande la barafu”.
Kuhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini amesema “uvumilivu wa vyama vya siasa ni jambo la msingi sana katika kulinda amani ya nchi”. Amesema ni lazima taifa lijifunze kujadiliana bila kupigana na kupingana kwa sera na hoja pasina kupigana na kuchochea uvunjifu wa amani.
Kwa upande wa rushwa na ufisadi, Waziri Mkuu mstaafu amesema “penye rushwa mwenye haki hunyimwa stahili yake na asiye na haki hununua haki ya mwingine”. Amesema kuwa rushwa hupofusha macho ya wanaoona na ni adui wa haki.
Awali akitoa taarifa fupi ya kituo hicho, Mratibu wa shirika la Children Care Development Organization (CCDO) Sixtus Kanyama amesema kuwa lengo kuu la shirika lake ni kuimarisha uwezo wa jamii katika kukuza elimu, afya na kutoa msaada wa kimaeneleo kwa jamii kupitia mafunzo ya teknolojia ya habari na mawasiliano (ICT). Amesema kituo hicho kitatoa mafunzo ya teknolojia kwa watoto kuanzia shule ya awali, msingi na sekondari na lugha za kigeni za kiingereza, kichina, kifaransa, kijerumani na kiarabu. Kituo hicho kwa kuanzia kinatarajiwa kugharimu shilingi milioni 120.  

Wednesday, May 18, 2011

ZAIDI YA BIL NNE ZAKUSANYWA KUTOKA VYANZO VYA NDANI IRINGA

Serikali za Mitaa mkoani Iringa zimefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni nne kutokana na vyanzo vyake vya ndani (own sources).

Akiwasilisha taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo na bajeti kwa mwaka 2010/ 2011 na mapendekezo ya mpango wa matumizi ya muda wa kati na bajeti (MTEF) mwaka 2011/ 2012- 2013/2014, Katibu Tawala Msaidizi- Sehemu ya Mipango na Urabitu, Nuhu Mwasumilwe amesema katika kipindi cha mwaka 2010/2011 Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa zilitarajia kukusanya jumla ya shilingi 7,051,034,698.00 kutokana na vyanzo vyake vya ndani.
Aidha, hadi kufikia mwezi Machi, 2011 jumla ya shilingi 4,476,848,601.96 zimekusanywa ambazo ni sawa na asilimia 63 ya lengo.

Kuhusu mapokezi na matumizi ya fedha zilizodhinishwa mwaka 2010/ 2011, Mwasumilwe amesema kuwa mwaka 2010/2011, mkoa wa Iringa uliidhinishiwa kutumia jumla ya shilingi 142,573,623,000.00 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo.

Aidha, kati ya hizo shilingi 105,256,869,000.00 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi 37,316,754,000.00 kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Hadi kufikia mwezi Machi, 2011 mkoa umetumia jumla ya shilingi 78,469,247,154.70 ambazo ni sawa na asilimia 81 ya fedha iliyopokelewa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo.

WIZARA YAANZISHA MPANGO WA KUENDELEA UTALII NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeanzisha mpango kamambe wa kuendeleza sekta ya utalii nchini utakaohusisha rasilimali za utalii zilizopo.

Hayo yamesemwa na Deograsias Mdamu, Afisa Utalii Mkuu kutoka Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati akiwasilisha mada juu Sera ya Utalii na Mkakati ya kuendeleza Utalii nchini katika kikao cha Kamati ya Uchauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo leo.

Mdamu amesema “mpango huu ni mkakati unaoelekeza jinsi ya kuendeleza utalii nchini kwa kuzingatia rasilimali za utalii, maendeleo ya mifumo mbalimbali, vivutio vikuu vya utalii, masoko ya utalii, taaluma ya kuhudumia sekta ya utalii, sera, sheria, taratibu na miongozo iliyopo”.

Akifafanua mikakati ya kukuza utalii, Mdamu ameitaja kuwa ni kuendeleza mazao mapya ya utalii, kutafuta masoko mapya na kuimarisha masoko ya zamani pia kuimarisha utafiti katika eneo la utafiti.

Vilevile, kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji baina ya Wizara na Taasisi za Serikali zinazohusika na maendeleo ya sekta ya utalii pamoja na kuongeza mapato ya utalii kutokana na leseni za biashara, mikataba ya uwekezaji na kodi.
Mikakati mwingine ameitaja kuwa ni pamoja na kuhimiza ubora wa huduma kwa utalii kama afya, benki, usalama na mawasiliano.

Kuimarisha utekelezaji wa sheria za kazi na haki za binadamu katika sekta ya utalii.
Kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi baina ya sekta za uzalishaji wa bidhaa na huduma nyingine zitumikazo na sekta ya utalii na kupanua ushiriki wa sekta hizi katika biashara za utalii.

Afisa Utalii Mkuu, ameongelea pia mtawanyiko wa sekta ya utalii na kusema kuwa sekta hiyo ni kubwa na imetawanyika katika makundi anuai huku kundi kubwa likiwa ni wafanyabiashara wenye mitaji midogo huku kundi dogo sana likiwa ndilo lenye wafanyabiashara wenye mitaji mikubwa.

Aidha, ameupongeza mkoa wa Iringa kwa kuwa na Maafisa Utalii katika Halmashauri zake ukiwa ni mkoa pekee wenye maafisa hao katika kila Halmashauri na kuahidi kuwapa ushirikiano stahiki katika kuiendeleza sekta ya utalii nchini.

Sekta ya utalii huchangia katika kuzalisha ajira, mapato ya fedha za kigeni na maendeleo katika sehemu mbalimbali mijini na vijijini.    

Mil 226 ZATOZWA KWA MAGARI KUZIDISHA UZITO

Zaidi ya shilingi milioni 226 zimelipwa kama tozo la uharibifu wa barabara kwa wakala wa barabara Mkoa wa Iringa kutokana na magari kuzidisha uzito imefahamishwa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa matengenezo na ukarabati wa barabara kwa mwaka wa fedha 2010/ 2011 kwa kipindi kinachoanzia Julai 2010 hadi Machi, 2011 na mpango wa mwaka wa fedha 2011/ 2012, katika kikao cha Bodi ya barabara Mkoa wa Iringa, Meneja wa wakala wa barabara (Tanroads) Mkoa wa Iringa, Mhandisi Paul Lyakurwa amesema katika kipindi cha Julai, 2010 hadi Machi, 2011 magari yaliyopimwa katika mizani isiyohamishika iliyopo katika mji mdogo wa Makambako ni 19,104 na kati ya magari hayo magari 2,494 (sawa na asilimia 13) yalizidisha uzito na kulipishwa tozo la uharibifu wa barabara kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Barabara Na. 30 ya mwaka 1973 na Kanuni zake za mwaka 2001 ambapo jumla ya shilingi milioni 226.582 zililipwa .

Meneja wa wakala wa barabara mkoani hapa amekemea vikali tabia inayoendelea kila kukicha ya matumizi mabaya ya hifadhi ya barabara kwa baadhi ya wananchi kuendea kufanya shughuli mbalimbali zikiwemo za kilimo na biashara ndani ya hifadhi ya barabara jambo linalosababisha kuziba kwa mifereji na makalavati na kusababisha maji kutuama barabarani na kusababisha harufu mbaya na magonjwa ya mlipuko. 

Baadhi ya Wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Iringa 


Baadhi ya Wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Iringa 

Aidha, amesema kuwa ofisi ya meneja wa wakala wa barabara mkoa wa Iringa inalo jukumu la kudhibiti uzito wa magari barabarani kwa kutumia mizani isiyohamishika iliyopo katika mji mdogo wa Makambako, Wilayani Njombe.
AHADI ZA DR. JK ZAANZA KUTEKELEZWA NA TANROADS IRINGA

Ofisi ya Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Iringa (TANROADS) imeanza utekelezaji wa ahadi za Mhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010 kuhusu sekta ya barabara mkoani hapa.

Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Iringa,
Mhandisi Paul Lyakurwa

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ahadi hizo katika kikao cha Bodi ya Barabara ya mkoa wa Iringa kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo, meneja wa wakala wa barabara (TANROADS), Mhandisi Paul Lyakurwa amesema ujenzi wa barabara ya Iringa-Mtera-Dodoma yenye urefu wa Km 260 kwa kiwango cha lami umeanza.

Amesema utekelezaji wa mradi huo umegawanyika katika sehemu tatu za Iringa-Migoli (Km 95.2), Migoli- Fufu (Km 93.2) na Fufu- Dodoma (Km70.9).
Aidha, mkataba kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Iringa-Migoli (95.2)  ulisainiwa tarehe 13 Januari, 2011 kati ya TANROADS na Mkandarasi M/S China Sichuan International Cooperation Co. Ltd kwa gharama ya Tshs. 84,216,378,355.50 wakati muda wa kukamilisha kazi ni miezi 35. Sehemu ya Migoli-Fufu (93.2) mkataba ulisainiwa tarehe 13 Januari, 2011 kati ya TANROADS na Mkandarasi M/S China Sichuan International Cooperation Co. Ltd kwa gharama ya Tshs. 73,612,329,958.67 wakati muda wa kumaliza kazi ni miezi 35. Sehemu ya Fufu-Dodoma (Km 70.9) mkataba ulisainiwa tarehe 13 Januari, 2011 kati ya TANROADS na Mkandarasi M/S China Communication Construction Co. Ltd kwa gharama ya Tshs. 64,327,389,129 wakati muda wa kukamilisha kazi ni miezi 27 na mkandarasi anaendelea na ujenzi wa kambi.

Kuhusu kukamilisha ujenzi wa barabara ya Njombe- Makete yenye urefu (Km 109) kwa kiwango cha lami, Meneja wa TANROADS amesema kuwa ujenzi wa Km 9.5 kati ya Mang’oto na Tandala ndani ya Wilaya ya Makete umekamilika. Aidha, ujenzi wa Km 2 maeneo ya Mang’oto unaendelea na unatarajia kukamilika ndani ya mwaka wa fedha 2010/2011.

   Aseri Msangi, Mwenyekiti (wa pili kulia), Gertrude Mpaka, Katibu (wa pili kushoto), Dr. Binilith Mahenge, Makamu Mwenyekiti (wa kwanza kulia) na Deo Sanga, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa (wa kwanza kushoto)

Akiongelea mpango uliopo kwa mwaka 2011/ 2012 Meneja huyo ameutaja kuwa ni kufanya upembuzi yakinifu, usanifu pamoja na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara yote kwa kiwango cha lami kama fedha zitapatikana.

Kuhusu maeneo korofi amesema yataendelea kuimarishwa kwa changarawe ili barabara iendelee kupitika kipindi chote cha mwaka.

Wednesday, May 4, 2011

PONGEZI KWA VYOMBO VYA HABARI IRINGA



Vyombo vya habari vya Mkoa wa Iringa vimepongezwa kwa jitihada kubwa vinazozifanya za kuhamasisha michezo Mkoani hapa hususani mpira wa miguu.
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka wakati akipokea shilingi 1,500,000 fedha taslimu zikiwa ni ufadhili wa kampuni ya bia Tanzania (TBL) kwa timu ya Mkoa wa Iringa katika mashindano ya Kili Taifa Cup mwaka 2011 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa leo.
Mwakilisi wa TBL Mkoani Iringa, Masumbuko John Changwe (katikati) akimkabidhi 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka (kulia) Tshs. 1,500,000 za ufadhili
wa timu ya Mkoa wa Iringa, kushoto ni Afisa Michezo Mkoa Keneth Komba
akishuhudia tukio hilo.

Akitoa shukrani hizo Bibi. Mpaka amesema “nawashukuru sana kampuni ya bia Tanzania kwa mchango wenu wa fedha na vyombo vya habari kwa jitihada kubwa za kuhamasisha michezo na kuutangaza Mkoa wa Iringa”.
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa ambaye ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Mkoa amewaasa wanamichezo wanaouwakilisha Mkoa wa Iringa katika mashindano ya Kili Taifa Cup kuzingatia nidhamu ya hali ya juu ili waweze kuuletea Mkoa ushindi na heshima kubwa.
Bibi. Mpaka amesema kuwa Serikali inathamini sana michezo na kukuza vipaji vya wanamichezo nchini na kutokana na umuhimu huo ndio maana Serikali imerudisha michezo ya UMITASHUMTA na UMISETA shuleni.
Awali akitoa maelezo kabla ya kukabidhi fedha za ufadhili wa TBL, mwakilishi wa TBL Mkoani Iringa, Masumbuko John Changwe amesema kuwa kampuni ya bia nchini inamalengo ya kuinua vipaji vya wanamichezo vijana nchini na kuwapatia ajira kupitia michezo.
Aidha, amekemea vikali vitendo visivyo vya kimichezo vya kuwapiga waamuzi na matumizi ya lugha ya matusi kwa wanamichezo. Vilevile amesisitiza kuwepo kwa mfumo mzuri wa kupata timu ya Mkoa iliyo bora kwa kuwashirikisha wadau wote ili timu ya Mkoa iwe na sura ya kimkoa.       
 Nae Katibu wa chama cha mpira wa miguu mkoani hapa Eliud Mvella amesemakuwa changamoto iliyopo ni udhamini ambapo amesema kuwa chama chake kipo mbioni kufanya maongezi na kampuni ya bia Tanzania ili waongeze wigo wa fedha katika udhamini wao.
Timu ya mpira wa miguu ya Mkoa wa Iringa itaondoka kesho tarehe 5 Mkoani hapa kuelekea kuelekea Mkoani Mbeya ambapo inajiwinda kufungua dimba na timu ya Mkoa wa Mbeya hapo tarehe 7 Mei, 2011.

MATUKIO YA MEI DEI KATIKA PICHA

Mgeni rasmi akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala Mkoa,Alhaji Adam Swai



Mgen rasmi akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala Msaidizi,
Sehemu ya Menejimenti ya Serikali za Mitaa, Sifael Kivamba


Mgeni rasmi akisalimiana na Mkuu wa Itifaki, Bahati Golyama

 Mgeni rami akisalimiana na Katibu Tawala Wilaya ya Iringa, Gideon Mwinami


 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Alhaji Mwamwindi akisalimiana na
Katibu Tawala Wilaya ya Iringa, Gideon Mwinami

 Baadhi ya Wafanyakazi Hodari wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Neema Mwaipopo na Vicent James

Waandamanaji katika MEI DEI

...Zingatieni kanuni za kazi
Waajiri wametakiwa kuzingatia misingi na kanuni za kazi ili kuweza kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza kwa kukiukwaji huo mahala pa kazi.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evarista Kalalu katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani- Mei Mosi iliyofanyika kimkoa Wilayani Mufindi leo.


Kaimu Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa (kushoto), Mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika maadhimisho ya Meimosi, Evarista Kalalu (katikati) na kuu wa Wilaya ya Ludewa, Georgina Budala (kulia)

Kaimu Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa (kushoto), Mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika maadhimisho ya Meimosi, Evarista Kalalu (katikati) na kuu wa Wilaya ya Ludewa, Georgina Budala (kulia)

Kalalu amesema “ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima mahala pa kazi waajiri wote wafanye kazi kwa kufuata misingi ya Sheria na Kanuni za kazi”. Mfanyakazi anawajibu wa kuipenda kazi yake lakini kero za kikazi zinapokuwa nyingi humfanya mfanyakazi kuichukia na ufanisi wa kazi yake kupungua. “Naomba sana tujitahidi kupunguza kero kwa wafanyakazi wetu na ikibidi tuwape motisha ambazo zitawafanya wafanye kazi kwa bidii” amesisitiza Kalalu.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Mufindi amewata waajiri kuwa makini wanaposhughulikia utatuzi wa kezo za wananchi kuzingatia makundi yote husika. Amesema kutokufanya hivyo kunaweza kujenga mianya ya kutengeneza makundi baina ya wafanyakazi na badala ya kutatua kezo husika kujikuta wanatengeneza kero na migogoro mingine ambayo ingeweza kuepukika.
  
Aidha, amewataka waajiri kutenga  muda wa kukaa na waajiriwa wao ili kujadili masuala mbalimbali ya kazi na matatizo yanayojitokeza ili yamalizwe kwa njia ya mazungumzo.

Awali akisoma risala ya wafanyakazi wa Mkoa wa Iringa, Mratibu wa TUCTA Mkoa, Khatibu Juma Baweni amesema kuwa wafanyakazi wanawajibu wa kufanya kazi kwa bidii na kuongeza tija katika jitihada za kuongeza pato la taifa. Amesema “kila mtu akitimiza wajbu wake hapatakuwa na malalamiko baina ya wafanyakazi na waajiri” amesisitiza Baweni. Aidha, amesisitiza kilio cha wafanyakazi dhidi ya kupanda kwa bei ya umeme, mafuta na bidhaa nyingine jambo lisiloenda sanjali na upandaji wa mishahara ya wafanyakazi jambo linalomdidimiza mfanyakazi kiuchumi.

Maadhimisho haya ya siku ya wafanyakazi duniani maarufu kama Mei Mosi ni kumbukumbu ya mapambano ya wafanyakazi ya kujikomboa yaliyoanzia Ulaya na Marekani ya Kaskazini katika karne ya 18 na 19 kutoka katika ukandamizaji na unyonyaji wa waajili kutokana na ukuaji wa viwanda.   







Monday, March 14, 2011


SOMA, Japan – Radiation is spewing from damaged reactors at a crippled nuclear power plant in tsunami-ravaged northeastern Japan in a dramatic escalation of the 4-day-old catastrophe. The prime minister has warned residents to stay inside or risk getting radiation sickness.

Chief Cabinet Secretary Yukio Edano said Tuesday that a fourth reactor at the Fukushima Dai-ichi complex was on fire and that more radiation was released
Prime Minister Naoto Kan warned that there are dangers of more leaks and told people living within 19 miles (30 kilometers) of the Fukushima Dai-ichi complex stay indoors.

Nuclear Power Plant

THIS IS A BREAKING NEWS UPDATE. Check back soon for further information. AP's earlier story is below.
TOKYO (AP) — Japan's nuclear safety agency said an explosion Tuesday at an earthquake-damaged nuclear power plant may have damaged a reactor's containment vessel and that a radiation leak is feared.

The nuclear core of Unit 2 of the Fukushima Dai-ichi nuclear plant in northeast Japan was undamaged, said a spokesman for the Nuclear and Industrial Safety Agency, Shigekazu Omukai.

The agency suspects the explosion early Tuesday may have damaged the reactor's suppression chamber, a water-filled tube at the bottom of the container that surrounds the nuclear core, said another agency spokesman, Shinji Kinjo. He said that chamber is part of the container wall, so damage to it could allow radiation to escape.

"A leak of nuclear material is feared," said another agency spokesman, Shinji Kinjo. He said the agency had no details of possible damage to the chamber.
Radiation levels measured at the front gate of the Dai-ichi plant spiked following Tuesday's explosion, Kinjo said.

Detectors showed 11,900 microsieverts of radiation three hours after the blast, up from just 73 microsieverts beforehand, Kinjo said. He said there was no immediate health risk because the higher measurement was less radiation that a person receives from an X-ray. He said experts would worry about health risks if levels exceed 100,000 microsieverts.

Picha ya chini ni Mripuko kwenye viwanda mjini Sendai
Mripuko kwenye viwanda mjini SendaiBildunterschrift:
 

Japanese ordered indoors in radiation leak crisis