Wednesday, September 13, 2017

VYOMBO VYA HABARI VYATAKIWA KUTANGAZA UTALII KARIBU KUSINI



Na Mwandishi Maalum, Iringa
Vyombo vya habari katika mikoa ya nyanda za juu kusini vimetakiwa kutangaza maandalizi ya maonesho ya Utalii Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda ili kuwaletea maendeleo wananchi wa kanda hiyo.

Wito huo ulitolewa na mwenyekiti wa kikao cha viongozi wakuu wa mikoa ya nyanda za juu kusini katika maandalizi ya maadhimisho ya maonesho ya Utalii Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo (SIDO), mheshimiwa Amina Masenza katika kikao kilichofanyika hifadhi ya taifa ya Ruaha jana.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza

Mheshiniwa Masenza ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Iringa alisema kuwa vyombo vya habari katika mikoa ya nyanda za juu kusini vina mchango mkubwa katika kufanikisha maonesho ya Utalii Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo (SIDO). 

Waandishi wa habari mna jukumu muhimu katika kufanikisha shughuli hii. Nawaomba mtusaidie kutangaza Utalii Karibu Kusini na shughuli za viwanda vidogo” alisema mheshimiwa Masenza.

Wakuu wa mikoa ya nyanda za juu kusini walioshiri ziara hiyo ni mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mkuu wa Mkoa wa Songwe na mkuu wa mkoa wa Njombe.

Maonesho ya Utalii yatafanyika pamoja na Maonesho shughuli za Viwanda Vidogo (SIDO) kanda ya nyanda za juu kusini kwa Mwaka 2017.  Maonesho haya yamepangwa kufanyika kuanzia tarehe 29/09/2017 hadi tarehe 02/10/2017.
=30=

No comments:

Post a Comment