Sunday, October 1, 2017

IRINGA KITOVU CHA UTALII NYANDA ZA JUU KUSINI



Na Mwandishi Maalum, IRINGA
Mkoa wa Iringa ni kitovu kikuu cha kuendelea utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini kwa mujibu wa mipango ya wizara ya Maliasili na Utalii ya kuendeleza utalii nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe wakati wa kufungua maadhimisho ya siku ya utalii Duniani, maonesho ya Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo (SIDO) mjini Iringa jana.

Prof. Maghembe alisema “napenda kuchukua fursa hii kuendelea kuwakumbusha mipango yetu juu ya maendeleo ya utalii ukanda wa kusini. Kwa mujibu wa mpango kabambe wa kuendeleza utalii nchini wa mwaka 2002 (integrated Tourism Master Plan 2002), Iringa ni kituo kikuu (hub) ya maendeleo ya utalii ukanda wa kusini”. Aliongeza kuwa tayari juhudi za kufanikisha jambo hilovzinaendelea vizuri. 

Kupitia mradi resilient natural resources management for growth, pamoja na mambo mengine tunalenga kuimarisha miundombinu ya ndani ya hifadhi, kuboresha vivutio vya utalii, kuhamasisha uwekezaji wa biashara za utalii kuimarisha utangazaji, kujenga ofisi ya wizara ya kanda” alisema Prof. Maghembe.

Nae mkuu wa mkoa wa Iringa, mheshimiwa Amina Masenza alisema kuwa mkoa wake daima utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha sekta ya utalii inakuwa ya mfano na kukua kwa kasi.
=30=

No comments:

Post a Comment