Sunday, October 1, 2017

MAONESHO YA UTALII KARIBU KUSINI NA SIDO KUTANGAZA FURSA



Na Mwandishi Maalum, IRINGA
Maonesho ya utalii karibu kusini na wajasiriamali wa SIDO yatumike kutangaza shughuli, fursa na vivutio vilivyopo mikoa ya nyanda za juu kusini.

Kauli hiyo ilitolewa na waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe wakati wa kufungua maadhimisho ya siku ya utalii Duniani, maonesho ya Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo (SIDO) mjini Iringa jana.
Prof. Jumanne Maghembe

Prof. Maghembe alisema “kipekee nimefurahishwa na maonesho ya karibu kusini mwaka 2017 ambayo kwa mwaka huu yamejumuisha wajasiriamali wa SIDO ambao ni wazalishajai wa bidhaa mbalimbali zinazoweza pia kutumiwa na watalii na kutoa huduma za kitalii nchini. Karibu kusini ni fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika mikoa ya nyanda za juu kusini na kuhamasisha wananchi na wadau mbalimbali kutembelea vivutio hivyo”. 

Aliongeza kuwa nchi ya Tanzania ina maeneo mengi yenye fursa za uwekezaji ambazo hazijaendelezwa ipasavyo.

Aliyataja maeneo hayo kuwa ni ukanda wa nyanda za juu kusini wenye vitutio vingi na vizuri vya utalii wakiwemo wanyama pori. Vivutio vingine alivitaja kuwa ni hifadhi za misitu asili, mandhari nzuri za kuvutia, bonde la usangu na mto ruaha, ziwa nyasa na kimondo. 

Vivutio hivi hutoa fursa na kuendeleza utalii katika ukanda huu. Aidha, ni wakati muafaka wa kuzitangaza fursa hizi ili kuvutia wawekezaji waje kuwekeza katika ukanda huu” alisema Prof. Maghembe.

Nae mkuu wa mkoa wa Iringa, mheshimiwa Amina Masenza alisema kuwa mkoa wake daima utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha sekta ya utalii inakuwa ya mfano na kukua kwa kasi.
 =30=

No comments:

Post a Comment