Thursday, August 9, 2012

WILAYA ZATAKIWA KUJIFUNZA KILOLO


Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita ametoa wito kwa wilaya nyingine kuitembelea wilaya yake kwa lengo la kujifunza mikakati inayowawezesha kulima kwa ubora na uhifadhi wa mazingira.
Kauli hiyo ameitoa alipofanya mahojiano na gazeti hili katika banda la Wilaya ya Kilolo lililopo katika uwanja wa Maonesho wa John Mwakangale Uyole, Jijini Mbeya.

Guninita amesema kuwa wilaya yake imegawanyika katika ukanda wa juu unaohusisha tarafa ya Kilolo wenye miinuko na mabonde jambo linalofanya ugumu katika matumizi ya zana bora za kilimo kama powatila na matrekta.

Amesema ukanda wa chini wenye tarafa za Mazombe na Mahenge una maeneo ambayo ni tambarare pamoja na kuwa na ukame maeneo hayo yanafaa kwa matumizi ya zana bora za kilimo yakiwemo matrekta.

Guninita amesema pamoja na changamoto hiyo ya kijiografia na mabadiliko ya tabia nchi, bado wilaya yake inajivunia utaratibu wa wananchi wake wa kutunza mazingira hasa utunzaji wa vyanzo vya maji. Amesema utunzaji huu wa vyanzo vya maji una mchango mkubwa katika shughuli za kilimo jambo linalowawezesha wakulima wa wilaya hiyo kuweza kulima kwa mwaka mzima. Ameyataja mazao yanayolimwa zaidi kuwa ni maharage, njegere, mahindi, mbogamboga, magimbi, muhogo, na viazi mviringo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo amesema kuwa wilaya yake imefanikiwa katika uhifadhi wa mazingira kwa uongozi wa wilaya kwa kushirikiana na wadau wengine kuwekeza katika elimu ya uhifadhi wa mazingira. Amesema katika ziara zake za kutembelea wilaya yake baada ya uteuzi wake mapema mwaka huu, katika kata zote 22 alizotembelea amekuwa akisisitiza utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa vyanzo vya maji. Aidha, wananchi wamehamasishwa kuacha vitendo vya uchomaji moto miti ya asili na misitu ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mkakati mwingine ameutaja kuwa ni wananchi kuhamasishwa katika ulinzi shirikishi unaohusika katika kulinda misiti na hifadhi ya mazingira. Amesema “katika hili la uhifadhi wa mazingira baada ya kutoa elimu na hamasa wale wote watakaobainika watafikishwa katika mkondo wa sheria. Tumekuwa tukisisitiza sana Sheria ya Uhifadhi wa Mazingira ya mwaka 2004, inayotoa adhabu isiyopungua sh. 2,000,000, kifungo cha miaka mitatu au vyote kwa pamoja.

Akiongelea tuzo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya utunzaji wa Mazingira kwa wilaya yake ya kilolo, Guninita amesema “katika kudhihirisha tabia ya uhifadhi wa mazingira kwa wilaya ya Kilolo, wilaya yetu imekuwa mshindi wa kwanza kitaifa. Kata ya bora ni Bomalang’ombe na taasisi bora imetoka katika wilaya yetu nayo ni gereza la Kihesa Mgagao”.

Amesema tuzo hiyo ya Rais, imeendelea kuamsha ari kwa wilaya yake, kuendelea kuhamasisha upandaji miti na uhifadhi wa mazingira. Ameitaja kampuni ya New Forest kuwa nayo inachangia kutoa hamasa kwa wananchi ya kupanda miti kwa wingi na kujiongezea kupato.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa katika kuhakikisha mkulima wa Kilolo anaendelea kuwa na lishe nzuri, wilaya yake imeendelea kuhamasisha ufugaji wa ng’ombe wa maziwa. Amesema katika kuhakikisha ufugaji wa ng’ombe wa maziwa unashika kasi, wananchi wamehamasishwa kuzitumia rasilimali walizonazo kufuga kisasa na ufugaji wenye tija. Amesema ufugaji wa kisasa na wenye tija ni ule wa ng’ombe wachache ambao mfugaji anaweza kuwahudumia vizuri na kuepuka mfugaji kuwa mtumwa kwa ngo’mbe wake.

Amesema Halmashauri yake kupitia DADPs imekuwa ikifanya vizuri katika hilo na ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma imeamsha ari zaidi ya ufugaji wa ng’ombe wa maziwa wilayani hapo.
=30=

KILIMO HAI KIPEWE MSISITIZO ZAIDI



Wakulima wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wameshauriwa kutumia kilimo hai katika kujihakikishia uhai wa mazingira na usalama wa chakula kwa kukuza kipato na kupunguza gharama za uwekezaji katika kilimo.

Ushauri huo umetolewa na Lawrence Mgora, mkulima mwezeshaji wa kilimo hai kutoka taasisi ya uenezi wa elimu ya ugani na kilimo hai.

Akiongelea maana ya kilimo hai amesema kuwa ni kilimo kinachoangalia uhai wa mazingira, uhakika na usalama wa mlaji na usalama wa chakula jambo ambalo linamuhakikishia mkulima kipato kwa kutumia fursa alizonazo mkulima.

Mgora amesema kuwa ili kilimo kiwe kilimo hai ni lazima ulimaji wake ufuate kanuni za kilimo hicho. Amezitaja kanuni hizo kuwa ni pamoja na matumizi ya mbolea ya asili kama mchuzi wa mmea, uji wa mmea na lishe ya mmea katika uzalishaji wa mazao kwa kupandia na kukuzia. Kanuni nyingine amezitaja kuwa ni dawa za asili katika kudhibiti mmea shambani na katika hifadhi ya mazao pamoja na tiba asilia kwa mifugo wa aina yote. 

Akiongelea kwa mifano hai mafanikio ya kilimo hai kwa mkulima na jamii, Mkulima mwezeshaji huyo ameyataja kuwa ni kuongezeka kwa mapato kwa heka. Amesema kuwa kwa mujibu wa tafiti walizofanya, mavuno ya mahindi yanayopatikana ni magunia 34 kwa heka kwa kutumia kanuni za kilimo hai ukilinganisha na magua 18 kwa kutumia kilimo cha kisasa. Ameongeza kuwa uzito wa mazao nao huongezeka, kwa debe la mahindi lililolimwa kwa kanuni za kilimo hai huwa na uzito wa kilo 22 ukilinganisha na kilo 18 kwa debe la mahindi lililolimwa kisasa. Akiongelea uhufadhi wa mazingira, amesema kuwa kilimo cha kisasa uharibu udongo jambo linalomlazimu mkulima kutumia mbolea mara kwa mara wakati kilimo hai kinahifadhi mazingira.

Akielezea nafasi ya ushirika katika kumsaidia mkulima wa Wilaya ya Kilolo, Afisa Uhirika Wilaya, Biezel Malia, amesema kuwa ushirika katika wilaya ya Kilolo umekuwa unalenga katika kumuwezesha mkulima kupata masoko ya mazao na mitaji kupitia Saccos na taasisi za kifedha. Amesema pia kupitia ushirika wilaya ya Kilolo imeweza kuwahakikishia wakulima upatikanaji wa pembejeo za kilimo na zana za kilimo kama pawatila, matrekta.

Amesema pamoja na juhudi za wilaya kuwawezesha wakulima kupata mikopo kupitia Saccos na taasisi za kifedha, ipo changamoto ambayo wanachama wengi sio waaminifu katika kurejesha marejesho ya mikopo yao. Aidha, amesema kuwa changamoto nyingine ambayo wilaya yake inaifanyia kazi ni uhamasishaji juu ya umuhimu wa kuweka akiba ili kuweza kukopa baadae. Afisa Ushirika huyo amesema kuwa katika kukabiliana na changamoto hiyo ngazi ya wilaya, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2012/2013 wilaya yake imetenga fedha za kutosha kutoa mafunzo ya kina kwa wakulima na wajasiliamali itakayoenda sambamba na elimu ya mikopo kwa wanachama wa Saccos.

Wilaya ya Kilolo ina aina nne ya vyama vya ushirika, vikiwepo vyama vya ushirika vya mazao (9), vyama vya akiba na mikopo (13), ushirika wa wapiga picha (1) na vyama vya wavuvi (2).
=30=

SERIKALI YABUNI MIKAKATI YA KUKUZA KILIMO



Serikali imeendelea kubuni na kutekeleza mikakati mbalimbli ya kwa lengo la kuhakikisha kuwa taifa linakuwa na chakula cha kutosha kwa wananchi wake na ziada kwa ajili ya watu wengine.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma katika kilele cha sikukuu ya wakulima na maonesho ya Nanenane mwaka 2012 yaliyofanyika kikanda katika viwanja vya Maonesho ya kilimo vya John Mwakangale Jijini Mbeya.
 Mgeni rasmi katika kilele cha Maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Dr. Christine Ishengoma alipotembelea banda ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

Katika hotuba yake, Dkt. Christine amesema “katika jitihada za taifa letu za kujitosheleza kwa chakula, mikakati mbalimbali imeendelea kubuniwa na kutekelezwa ikiwa ni pamoja na kanda ya Nyanda za Juu Kusini kupewa jukumu la kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi na kuwa ghala la chakula la Taifa kutokana na fursa nzuri za uzalishaji zilizopo hatika mikoa hii”.

Amesema ili jukumu hili la kitaifa lifanikiwe ni lazima wakulima wazalishaji wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kutumia vizuri fursa zilizopo, kuzalisha kwa tija kwa kutumia kanuni bora za kilimo zitakazowawezesha kupata ziada ya chakula ya kuuza kwa mikoa mingine isiyokuwa na firsa nzuri za uzalishaji.

Akiongelea viwanzo tija vya uzalishaji wa mazao ya chakula, Dkt. Christine amesema “..viwango vya tija katika uzalishaji wa mazao ya chakula kwa eneo bado viko chini. Takwimu zinaonesha kuwa, katika Nyanda za Juu Kusini uzalishaji wa mahindi kwa mfano, ni kati ya tani 2-3 kwa hekta moja wakati ambapo utafiti unaonesha kwamba hekta moja inaweza kuzalisha hadi tani 7”.Aidha, ametoa wito kwa viongozi na wakulima kuyatumia maonesho hayo kama jukwaa la kuwajengea uwezo wazalishaji wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuongeza tija na kufikia uwezo wa juu katika uzalishaji kadri inavyowezekana.

Akiongelea ufugaji, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, amesema kuwa kanda hiyo ina fursa ya ufugaji kutokana na uwepo wa ardhi, mvua za kutosha, miundombinu ya machinjio ya kisasa na rasilimali kubwa ya mifugo. Amesema mifugo imekuwa ikichangia katika uzalishaji wa mazao ya kilimo kwa njia ya nguvu kazi na samadi. Amesema “katika kanda hii, asilimia 70 ya wakulima hutumia wanyamakazi katika shughuli za kilimo. Hii ni hatua kubwa inayostahili kupongezwa kwani matumizi ya nguvukazi ya wanyama ni moja kati ya teknolojia rahisi, sahihi na endelevu kwa wakulima wetu”.

Ikumbukwe kuwa sekta ya kilimo nchini inatoa ajira kwa karibia asilia 80. Vilevile, wakazi karibu asilimia 90 wa kanda ya Nyanda za Juu Kusini wanategemea kilimo kama shughuli kuu ya kiuchumi kwa mazao ya chakula na biashara.

=30=

MPAKA AWATAKA MPANDA KUPANDA MITI




 Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka ameshauri upandaji wa miti kwa wingi sana ili kuepukana na tatizo la wilaya hiyo kugeuka jangwa kutokana na matumizi makubwa ya kuni katika kukausha zao la tumbaku linaloendelea kushamiri katika wilaya ya Mpanda mkoa mpya wa Katavi.

Ushauri huo ameutoa alipotembelea banda la wilaya ya Mpanda katika uwanja wa maonesho ya Nanenane wa John Mwakangale- Uyole Mbeya.

Gertrude amesema kuwa kutokana na matumizi makubwa ya kuni zinazotumika katika kukaushia zao la tumbaku, ni vizuri wilaya hiyo ikajipanga katika kupanda miti kwa wingi ili kuziba pengo la miti inayokatwa kwa ajili ya matumizi ya kuni katika kukaushia tumbaku. Amesema kuwa ni vema mkakati huo ukaanza mapema wakati njia mbadala ya nishati ya ukaushaji wa tumbaku ikiangaliwa ili kutokuteketeza misitu na mazao yake.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda 

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, amesema njia za kisayansi zinahitajika katika kukausha majani ya tumbaku pasipo kuharibu mazingira. Aidha, ametoa wito wananchi kufikiria njia ya kiteknolojia itakayotumika katika ukaushaji wa majani hayo. Amesema kwamujibu wa kaulimbiu ya maonesho ya Nanenane mwaka 2012 isemayo “Kilimo kwanza, zalisha kisayansi na kiteknolojia kukidhi mahitaji ya ongezeko la idadi ya watu” vivyo hivyo wilaya ya Mpanda ifikirie hamasa ya maendeleo ya kiteknolojia katika kulifanya zao la tumbaku kuwa na tija zaidi katika ustawi wa wananchi na mazingira kwa ujumla wake.

Gertrude amesema kuwa ili kwenda sambamba na kauli mbiu hiyo, ni vizuri wilaya hiyo ikatoa hamasa zaidi katika utengenezaji wa zana zitakazosaidia katika kukipeleka mbele kilimo. Amesema kuwa wapo vijana wengi wanaoibuka na ubunifu wao kwa kutumia teknolojia rahisi wanaohitaji kupewa msukumo na kuendelezwa ili kuweza kuleta mapinduzi katika kilimo na ufugaji.

Akiongelea changamoto inayowakabili wanawake wajasiriamali katika upatikanaji wa masoko, Katibu Tawala Mkoa wa Iringa ametoa wito kwa wanawake wajasiriamali kuungama pamoja na kuunganisha nguvu zao katika shughuli zao za ujasiliamali. Amesema masoko ni changamoto inayowakabili wakina mama wengi wajasiriamali, na kushauri pindi wanapokuwa katika vikundi ni rahisi kwao kuweza kupatiwa mafunzo ya mbinu za upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi.

Amesema umefika wakati kwa wanawake wa Nyanda za Juu kusini kuungana na kutumia fursa iliyopo sasa ya soko pana la Afrika ya Mashariki.
=30=

Sunday, August 5, 2012

WAKULIMA NA WASINDIKAJI WAWEZESHWE ASEMA RC IRINGA



Halmashauri za Wilaya na Manispaa zimeshauriwa kuwasaidia wakulima na wajasiliamali wasindikaji katika kuhakikisha bidhaa zao zinafikia viwango vya ubora vinavyotakiwa ili kujihakikishia soko la uhakika.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipotembelea mabanda ya wajasiliamali na wasindikaji katika maonesho ya Nanenane katika Uwanja wa John Mwakangale -Uyole Mbeya katika siku ya Iringa Day.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr. christine Ishengoma (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Fama Food Processing, Genovefa barnabas katika Uwanja wa Maonesho ya NaneNane Mbeya

Dkt. Christine amesema kuwa wakulima wasindikaji wanafanya kazi kubwa sana katika kusindika bidhaa za kilimo kwa kutumia juhudi zao wenyewe, hivyo kujikuta wakikwama katika utaalam na kushauri wawe wanapatiwa mafunzo na ushauri wa kitaalam ili kuufanya usindikaji wao uwe wa kisasa zaidi.

Amesema ni vizuri Halmashauri za Manispaa na Wilaya ziangalie jinsi ya kuwasaidia kitaalam na kiufundi ili bidhaa za usindikaji ziweze kufikia viwango vinavyokubalika na kupata lebo ya shirika la ubora (TBS). “watu wengi sasa wanaangalia lebo ya TBS ili kijihakikishia ubora hivyo ni vizuri mkahakikisha bidhaa zenu zinafikia ubora unaopkubalika na kupata lebo ya ubora” amesisitiza Dkt. Christine.

Akiongelea changamoto zinazowakabili wajasiliamali wasindikaji, mjasiliamali na mmiliki wa Fama Food Processing, Genovefa Barnabas amesema kuwa changamoto kubwa inayowakabili wajasiliamali hasa wa Mkoa wa Iringa ni maeneo mahususi ya kuwawezesha kuzalishia bidhaa zao ili ziweze kupata uthibitisho wa ubora unmaotakiwa.  Akifafanua zaidi amesema “ili mjasiliamali anu wajasiliamali tuweze kutimiza ndoto zetu za kufanya shughuli za ujasiliamali vizuri ni vizuri serikali ikatusaidia kutenga maeneo ambayo yatakuwa mahususi kwa shughuli za ujasiliamali ambapo kila kitu kitakuwa kinafanyika hapo”. Amesema “kuanzia mazao na bidhaa zinapoletwa kutoka maeneo mbalimbali zinapokelewa katika eneo hilo, zinaanza kutengenezwa katika eneo hilo, zinapakiwa katika kontena, kufungwa na kuwekwa lebo hapohapo, kwa lugha nyingine mchakato wote unafanyika katika eneo moja hadi kwenda kwa mlaji”.

Akitetea umuhimu wa eneo hilo kwa wajasiliamali, Barnabas amesema kuwa eneo hilo lina umuhimu mkubwa kwa sababu kupatikana kwake kutawawezesha kupata cheti cha ubora wa bidhaa toka shirika la viwango (TBS). Amesema kitendo cha kupata lebo ya ubora toka TBS kutawafanya watu wengi zaidi kujiridhisha na ubora wa bidhaa hizo.  

Nunu Mtatifikolo ambaye ni Mwenyekiti kikundi cha Wanawake cha JAFAKU amesema changamoto ya watanzania kukubali bidhaa zinazozalishwa na wajasiliamali wazalendo wa ndani ni mwiba katika ukuaji wao. “amesema ipo kasumba inayoendelea kutudidimiza ya wananchi kupenda bidhaa za nje tofauti na zinazozalishwa na wajasiliamali wa ndani”.

Amesema ili kuondokana na kasumba hiyo elimu inahitajika kutolewa kwa wananchi ili waweze kutumia bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi. “Elimu hiyo itasaidia sana kubadili kasumba hii na elimu hii inatakiwa kuambatana na matangazo ya bidhaa za wajasiliamali” amesisitiza Mtatifikolo.

Mwenyekiti wa kikundi cha Wanawake wa KKKT-Nduli, Laurencia Malila amesema katika banda la Manispaa ya Iringa amesema kuwa wanawake wajasiliamali Mkoani Iringa wanakabiliwa na changamoto ya masoko kwa maana ya wanunuzi wa bidhaa zao. Amesema “pamoja na kuwa na bidhaa nzuri bado wananchi wanamuitikio mdogo wa kuzinunua jambo linalowafanya washindwe kuzalisha bidhaa kwa wingi”.  

Malila ambaye pia kikundi chake kinajihusisha na kilimo cha kisasa na ufugaji wa nyuki kikiwa na mizinga 47 ya nyuki ya kisasa, ametoa wito kwa watu wanaopenda kujifunza kilimo cha kisasa cha mahindi na maharage pamoja na ufugaji wa nyuki kuwatenbelea ili kujifunza katika mashamba darasa yao yaliyopo katika kata ya Nduli.

=30=

DR. ISHENGOMA ASISITIZA KILIMO CHA KISAYANSI



Zana ya Kilimo Kwanza itafanikiwa kwa wakazi wa kanda ya Nyanda za Juu Kusini kulima kilimo cha kisayansi na kiteknolojia zaidi na kukifanya kilimo kiwe cha kibiashara.

Ushauri huo umetolewa katika majumuisho baada ya mgeni rasmi Dkt. Christine Ishengoma kutembelea mabanda ya maonesho ya Nanenane kanda ya nyanda za Juu Kusini katika siku ya mkoa wa Iringa (Iringa Day) iliyofanyika katika uwanja wa maonesho ya Nanenane wa John Mwakangale Uyole Mbeya.

Dkt. Chrisrine ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema “kimsingi kilimo kwanza ni Nyanda za Juu Kusini yaani Mikoa ya Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Rukwa na Katavi kwa kuwa mikoa hii ndio wazalishaji wakubwa nchini, hivyo huwezi kutenganisha Kilimo Kwanza na Nyanda za Juu Kusini”.  Amesema katika kuendeleza kilimo katika ukanda huo ni lazima kilimo kiwe cha kisayansi na kiteknolojia zaidi ili kuwawezesha wakulima kulima maeneo madogo lakini kwa kupata mazao mengi zaidi na yenye ubora unaotakiwa. Amesema kuwa wakulima wameendelea kupata hasara katika kilimo kwa kutokufuata kanuni za kilimo bora jambo linalowafanya waweke nguvu nyingi katika kilimo lakini matokeo wanayoyapata hayaendani na nguvi halisi waliyowekeza katika kilimo hicho. Aidha, ametoa wito kwa wataalam wa kilimo kuwa karibu zaidi na wakulima ili kuwafundisha waweze kuepukana na kilimo cha kizamani na kimazoea.
Hapa huitaji maelezo zaidi ya picha kujieleza yenyewe

Akiongelea kuhama kutoka katika kilimo kidogo kwa ajili ya kujitosheleza kwa chakula, amesema “umefika wakati sasa wa kuhama kutoka katika kilimo cha kawaida na kukifanya kilimo chetu kiwe cha kibiashara. “Na hili litawezekana pale tu tutakapokifanya kilimo chetu kuwa kilimo cha kisayansi zaidi” amesema Dkt. Christine.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Iringa amesema baada ya kutembelea mabanda ya maonesho mikoa yote inafanya vizuri. Amesisitiza kuwa ili maonesho hayo yawe mazuri zaidi ni vema maandalizi yake yakaanza mapema zaidi katika Halmashauri zote.

Akielezea nini amejifunza katika maonesho hayo, amesema kuwa amejifunza mambo mengi sana ambayo baadhi hakuwa akiyafahamu kabisa, baadhi amejikumbusha baada ya kupita muda mrefu tokea ayafahamu na kusema “maonesho yaha yamekuwa ni shamba darasa kwa watu wengi”. Baada ya kujionea ubunifu wa kiteknolojia kutoka kwa wananchi mbalimbali, ametoa wito kwa mikoa hiyo ya nyanda za juu kusini kuwaangalia wabunifu hao kwa jicho la pekee ili waweze kuwaendeleza zaidi na wao kunufaika na ubunifu wao. Amesema kuwa imani yake ni kwamba pale juhudi za pamoja zitakapowekwa hakika kilimo kitatoka katika hali yake ya sasa na kuwa bora zaidi.

Wakati huohuo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa ameweka rekodi katika maonesho hayo ya Nanenane baada ya kutembelea mabanda 40 ya maonesho kwa siku na kupokea maelezo na kuuliza baadhi ya maswali kwa waoneshaji mbalimbali.

=30=

RC IRINGA ALIPOTEMBELEA MABANDA YA 8 8 KATIKA UWANJA WA JOHN MWAKANGALE



 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr. Christine Ishengoma (mwenye sutu ya zambarau) akikagua zana alipotembelea Banda la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa


  Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr. Christine Ishengoma (mwenye sutu ya zambarau) akikagua Mambo ya Lishe alipotembelea Banda la Halmashauri ya manispaa ya Iringa


 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr. Christine Ishengoma (mwenye sutu ya zambarau) akipokea maelezo ya Malisho ya Mifugo


 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr. Christine Ishengoma (mwenye sutu ya zambarau) katika picha ya pamoja alipotembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa. 


Mama Kiula ajumuika na wadau katika kutembelea Maonesho ya Nanenane Mbeya

 Banda la Manispaa ya Iringa 

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr. Christine Ishengoma akisaini Kitabu cha Wageni katika banda la Manispaa ya Iringa

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr Christine Ishengoma akibadilishana mawazo na Mjasiliamali jasiri, Genoveva Barnabas

Dr. Ishengoma katika banda la ASAS  

 RC Iringa akikagua banda la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, kulia ni kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa


 Mkuu wa Mkoa wa Iringa  akikagua mabanda ya Maonesho kulia kwake ni Shenal Nyoni

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa akipokea maelekezo katika banda la Halmashauri ya Wilaya Wilaya ya Iringa

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dr. Christine Ishengoma akisaini Kitabu cha wageni katika banda la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

Dr. Christine Ishengoma akioneshwa note feki na noti halisi za 10,000.

Monday, July 30, 2012

KKKT IRINGA WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA SENSA




Washarika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, usharika wa Iringa Mjini wametakiwa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa mabadiliko ya uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kufanikisha uundwaji wa Katiba hiyo kwa kujumuisha mapendekezo ya watu wengi zaidi.

Wito huo umetolewa na mgeni rasmi Dkt. Christine Ishengoma katika harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa kanisa kuu la mtaa wa Wilolesi iliyofantik Katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzanaia, Usharika wa Iringa Mjini leo.

Dkt. Christine ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, amesema “ndugu zangu Washarika natoa rai kwenu kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha na kuwaeleza waumini wengine na wananchi kwa ujumla ili washiriki katika mchakato huu kwa kutoa elimu na hamasa”. Amesema “napenda kutoa wito kwenu wote kuwa huru kutoa maoni yenu Tume itakapopita katika maeneo na kukusanya maoni yenu”. 

Amesema kuwa baadhi ya wananchi wanalalamika kuwa Katiba ya sasa inamapungufu kadhaa, hivyo huu ndio wakati wao wa kutoa maoni yao ili hayo mapungufu yaweze kufanyiwa kazi na kuingia katika Katiba mpya. Amesema hili litafanikiwa pale tu, washarika na wananchi watakapojitokeza kwa wingi kutoa maoni yao pindi tume ya kukusanya maoni itakapopita katika maeneo yao. Amewataka kuwa makini katika kusikiliza tarehe na sehemu ambazo mikutano hiyo itakuwa ikifanyika ili waweze kuwasilisha maoni yao kwa tume hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka wananchi kuwa huru katika kutoa maoni yao na kuwahakikishia kuwa ukusanyaji wa maoni hayo hauhusiani na itikadi yoyote. Amesema ili Katiba hiyo mpya iwe ya mafanikio ni lazima maoni ya wananchi wengi yaweze kukusanywa na mafanikio hayo yanatokana tu, na wananchi kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao kwa tume hiyo.  
=30=

TAASISI ZA DINI ZATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO ILI KUFANIKISHA SENSA




Serikali Mkoani Iringa imeomba ushirikiano kutoka kwa viongozi wa dini katika kuhakikisha kuwa elimu ya kutosha na hamasa vinatolewa ili uelewa huo uwafikie waumini na wananchi wengi kwa ujumla.

Ombi hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akiendesha zoezi la harambee ya ujenzi wa kanisa kuu la mtaa wa Wilolesi mjini hapa katika ibada ya kwanza iliyofanyika katika kanisa kuu, usharika wa Iringa Mjini.

Dkt. Christine amesema kuwa Tanzania itafanya Sensa ya Watu na Makazi tarehe 26 Agosti, mwaka huu na kuendelea kwa takriban siku saba. Amesema “Sensa ya Watu na Makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua na kusambaza takwimu za kidemografia, kiuchumi na kijamii kuhusiana na Watu wote na Makazi yao katika nchi kwa kipindi maalum”. Amesema kuwa Sensa hiyo ni zoezi lenye lengo la kupata idadi ya watu wote katika nchi, kwa umri na jinsi, mahali wanapoishi, hali yao ya elimu, hali ya ajira, hali ya vizazi na vifo na hali ya makazi. 

Akiongelea malengo ya Sensa hiyo, Mkuu wa Mkoa amesema “Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 inalenga kutathmini utekelezaji wa Mipango yetu mikubwa ya Maendeleo ambayo imekuwa ikitekelezwa katika kipindi kilichopita. Mipango hiyo ni pamoja na Mkakati wa Kupunguza Umasikini na Kukuza Uchumi Tanzania na Mpango wa Kupunguza Umasikini Zanzibar”.

Akiongelea nafasi ya kanisa katika kufanikisha Sensa hiyo, Dkt. Christine amesema “napenda kuongelea nafasi ya Kanisa katika kuhakikisha Sensa ya Watu na Makazi inafanikiwa. Ni kweli kuwa Kanisa linalo jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa zoezi hili linafanikiwa kwa sababu takwimu hizo ndizo zitakazoiwezesha Serikali kutambua hali halisi na mahitaji halisi ya huduma zilipo katika maeneo yenu hivyo kuingizwa katika Mipango ya Maendeleo ya Taifa”. Amesema “kwa msingi huo, ninawaomba sana kuwahamasisha waumini na wananchi kwa ujumla ili wahesabiwe na wahesabiwe mara moja tu, ili takwimu zitakazokusanywa ziwe sahihi”.

Ameyataja mambo muhimu ya kutiliwa mkazo wakati wa kuwahamasisha washarika na wananchi kwa jumla kuwa ni tarehe ya Sensa, umuhimu wa Sensa na yatakayojiri wakati wa zoezi la kuhesabu watu. Sensa hiyo ya Watu na makazi inaongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Sensa kwa maendeleo, jiandae kuhesabiwa’.

Tuesday, July 24, 2012

PROF. J.A. MILLS AFARIKI DUNIA



Taarifa kutoka afisi ya rais zinasema kuwa alifariki ghafla baada ya kupelekwa hospitali siku ya Jumatatu usiku.
Prof. John Attah Mills
Kifo cha rais wa taifa la pili duniani kwa ukuzaji wa cocoa kimekuja wakati alikuwa anajiandaa kupogania tena urais.Msaidizi wake pia amethibitisha kufariki kwa kiongozi huyo.

Rais Prof. John Attah Mills ambaye husafiri mara kwa mara kwenda ng'ambo kwa matibabu alifariki muda mfupi baada y kupelekwa katika hospitali moja mjini Accra , Ghana.

Ni hivi majuzi tu rais huyo alisafiri hadi Marekani kwa kile kilichosemekana kwa ni uchunguzi wa kawaida wa afya yake.

Kwa muujibu wa katiba ya Ghana, Makamu wa Rais  John Dramani Mahama anatarajiwa kushikilia hatamu za uongozi hadi uchaguzi wa urais utakapofanywa.

Ghana ilikuwa inatarajiwa kwenda katika uchaguzi mkuu mwezi Disemba mwaka huu ambapo Prof. John Attah Mills alikuwa ametangaza nia yake ya kutetea uadhifa wake.

Wakati wa uongozi wake, uchumi wa Ghana uliimarika na demokrasia kupanuka zaidi.

" Ni kwa masikitiko makuu na kwa moyo mzito... Tunatangaza kifo cha ghafla cha rais wa jamhuri ya Ghana " taarifa iliyotumiwa shirika la Reuters kutoka ofisi ya rais ilisema.

Taarifa hiyo ilisema kuwa Rais Prof. Mills mwenye umri wa miaka 68 alifariki saa chache tu baada ya kupelekwa hospitali.

Hata hivyo hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Lakini msaidizi wake mmoja ambaye hakutaka kutajwa, alisema kuwa Rais Prof. John Attah Millis alisikika siku ya Jumatatu akilalamika kwa anaumwa.

Hali yake ilizorota na hatimae kufariki mapema siku ya Jumanne.
Prof. Mills , anajulikana kwa kuanzisha uchimbaji wa mafuta nchi Ghana.

Chanzo: BBC SWAHILI



 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA



MKOA WA IRINGA:
Simu Na.  026 2702191   
Fax    Na. 026 2700310
 
  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,
   S. L. P. 858,

   IRINGA



YAH: MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA TAREHE 25 JULAI, 2012.


Wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Wananchi wa Manispaa ya Iringa kwa ujumla mnatangaziwa kuwa Tarehe 25 Julai, 2012 kutafanyika Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa katika Uwanja wa Bustani ya Manispaa ya Iringa saa 2:00 Asubuhi.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa atakuwa Mgeni Rasmi katika Maadhimisho hayo.
Unatakiwa kuhudhuria katika Maadhimisho hayo muhimu kwa Kudumisha Historia ya Ukombozi wa Nchi yetu.



Imetolewa na:
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa
S.L.P 858
IRINGA


Thursday, July 19, 2012

SPEECH BY HIS EXCELLENCY, DR JAKAYA MRISHO KIKWETE, THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, ON THE OCCASION OF THE OFFICIAL OPENING OF THE ALMA SECRETARIAT OFFICE IN DAR ES SALAAM, 18TH JULY, 2012





Your Excellency, Ellen Johnson Sirleaf, the President of
       the Republic of Liberia;
Honorable Hussein Ali Mwinyi (MP), Minister of
     Health and Social Welfare;
Dr. Rufaro Chatora, Representative of the World
      Health Organization in Tanzania;
Members of the Diplomatic Corps;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen;

Once again it is my pleasure to welcome you, Madame President, to Tanzania. We thank you very much for accepting my invitation to visit us and agreeing to launch the African Leaders Malaria Alliance (ALMA) offices.

Ladies and Gentlemen;
As many of you know, Africa is the continent most affected by malaria. The disease accounts for 85 percent of malaria cases and 89 percent of malaria deaths worldwide, the majority being children under five years of age and pregnant women. Malaria also retards economic growth of the continent and over-burdens the already overstretched health care services in most African countries.  In fact, malaria has been estimated to cost Africa at least US Dollars 12 billion every year.  Despite these devastating effects of malaria, the scourge can be prevented, controlled and eventually eliminated in Africa.

It is for this reason that in September, 2009, some African leaders gathered at the United Nations Headquarters in New York, United States of America and decided to form an alliance to intensify the fight against malaria and ultimately end malaria-related deaths in Africa.  We formed a coalition to mobilize and coordinate our collective efforts as well as mobilize international support from nations, international organizations as well as institutions and persons of goodwill in the fight against malaria.  We formed the African Leaders Malaria Alliance, in short ALMA.   I was privileged and honoured to be the first Chairman of ALMA until January, 2012 when I handed over to my dear sister Her Excellency President Ellen Johnson Sirleaf of the Republic of Liberia who is our chief guest at this event today.

Your Excellency;
Since its inception, ALMA has been very instrumental in enhancing global partnership and mobilizing substantial resources to fight the scourge of malaria in Africa. As a result, many African countries have been able to scale up malaria interventions and reduce malaria related deaths and the social burden of the disease it engenders. One of the landmark achievements was the adoption of the ALMA Scorecard for Accountability and Action in September, 2011.  In fact, this new innovative way of tracking progress on key malaria indicators establishes transparency and accountability framework for rapid response to emerging issues and consolidates national data from multiple sources.

I would like to take this opportunity to thank all the African leaders for their commitment and efforts to fight malaria; and to all our partners for their immense contribution and support towards our noble goal of eradicating malaria-related deaths by 2015. I know our target is ambitious but doable if we scale up interventions on the fight against malaria. I commend our very able ALMA Secretariat, under the leadership of Madam Joy Phumaphi, for the good work of building the institution and coordinating our efforts. Without the dedicated services rendered by staff of the Secretariat, we would not be here today celebrating one of our achievements. Thank you very much Madame Joy, Saleemah, Dr. Halima, Melanie, Kwame, Samson and Mary for your wonderful service to our dear continent.

 And above all, ladies and gentlemen, I want to sincerely thank President Ellen Johnson Sirleaf for her leadership in steering the affairs of ALMA. Within a very short time, her vibrancy and visionary leadership have proven to be an asset in the fight against malaria in Africa. I am sure by the time her tenure ends, Africa will leap several steps forward in the fight against malaria. Tanzania will continue to support you and the work of ALMA until we attain our lofty objective.

Your Excellency;
Invited guests;     
Ladies and Gentlemen;

On behalf of the government of the United Republic of Tanzania, it is now my pleasure to hand-over new offices of the ALMA Secretariat here in Dar es Salaam. These offices are available to ALMA as a contribution of the government and the people of the United Republic of Tanzania to ALMA in recognition of its efforts in fighting Malaria in the continent.    
Finally, it is now my singular honor and privilege to welcome you Madame President to the podium to deliver your remarks and then launch the ALMA Secretariat offices here in Dar es Salaam.
Madam, welcome!

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete together with  the Liberian  Presdent Ellen Sirleaf Johnson pose for a group photograph with some dignitaries who attended the official opening ceremony of the ALMA offices in Dar es Salaam this morning.The ALMA offices are located at the institute of Medical Research NIMRI Headquarters  along Luthuli Avenue in Dar es Salaam.